TMA yawataka wakulima kufuatilia utabiri wa Hali ya hewa.


Wakulima nchini wametakiwa kufuatilia utabiri wa hali ya hewa ili waendane na kilimo cha kisasa badala ya kile cha mazoea.

Ushauri huwo umetolewa na meneja wa mamlaka ya hali ya Hewa Pemba Bishara  Rashid Mdoe huko katika viwanja vya maonesho chamnangwe Mkoa wa Kaskazini Pemba wakati akizungumza na waandishi wa habari.



Amesema ili wakulima waendelee kupata mavuno mazuri nilazima wabadilike kutoka kile kilimo ambacho niche asili na badalayake wajikite zaidi katika kilimo ambacho kinafuata miongo ambayo inatangazwa na mamlaka husika.

Aidha amewataka wananchi kufuatilia utabiri wa hali ya hewa unao tolewa ili kuendana na mazingira na kuepuka majanga yanayoweza kuepukika.

Hatahivyo ameto wito kwa wananchi kufika katika maonyesho  iliwapate kujifunza zaidi na kuwa walimu wazuri wabaadae.





Comments