Serikali yashauriwa kutoisaini sharia na mikataba ya kimataifa ambayo haiendani na Mila na silka za Kitanzania.


Image result for tamwaSerikali imeshauriwa  kutokuwa tayari kuisainhi sharia na mikataba ya kimataifa inayokuja nchini  ambayo haiendani na mila na silka zetu ili kuepusha kuongezeka  kwa matatizo mbali mbali ikiwemo janga la udhalilishaji.

Ushauri huo umetolewa na Wakili Abdulkari Mussa katika semina maalumu iliyowakutanisha watendaji wa taasisi mbali mbali za kiserikali na binafsi  iliyoandaliwa na chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania (TAMWA) juu ya kuzipitia sharia ndogo ndogo zilizopendekezwa kwa lengo la kupambanha na matendo ya udhalilishaji wa wanawake na watoto ambazo zitatumika katika shehia  zote hapa nhchinhi.

Wakili huyo amesema baadhi ya mikataba na sharia za kimataifa zinazokuja nchi haziendani na maadili yetu hivyo hupelekea kuongezeka kwa mmong’onhyoko wa maadili.

Akitolea mfano wa sharia na mikataba hiyo amesema  ni pamoja na sharia na mikataba ya kimataifa ianayotoa kinga kwa watoto jambo ambalo limewafanya watoto kuwa na uhuru mkubwa wa kutenda mambo wanayoyataka huku wazazi wao wakikosa uhuru wa kuwaazibu.

"Mimi nakumbuka zamani ilikuwa ukifanya kosa unacharazwa bakora vizur mpaka unajuta napengine unapigwa na watu tofauti lakinini saivi wapi mototo anaweza kukushtaki na mzazi ukaingia hatiani". amesema wakili huyo.

Akichangia katika kipengele kilichowagusa walimu wa madrasa kilichoeleza kuwa mwalimu kutopokelewa  anapotoka madrasa moja kwenda nyengine hadi nawe na waraka maalum kutoka kituo cha polisi ili kuonasha kuwa hajawahi kushtumiwa kwa makosa ya uhalifu  Afisa fatwa na utafiti kutoka ofisi ya Mufti Shekh  Said Ahmad Mohd amesema ipo haja kwa serikali kuwasomesha walimum wa madras na kuwapa vyeti ndipo wakafanye kazi ya kosomesha kama walivyo walimu wa skuli.

"Niwaombe Tamwa muandae mpango maalum kuiomba Seriakali kuwasomesha walimu wa madras ili na wao wawe na sifa zenye kutambulika kama walivyo walimu wa skuli hii itasaidiwa kuwapata walimu walio waaadilifu maana tunaona baadhi ya walimu hawa nao wanashtumiwa katika kashfa hii". amesema afisa huyo.

Sambamba na hayo amesema kutokuwepo kwa  kinga kwa watoa ushahidi  juu ya masuala ya udhalilishaji ndio sababu iliyopelekea  kuongezeka kwa rushwa muhali katika jamii.

Akiwasilisha sherea hizo ndogo ndogo wakili Walid Mohd Adam amesema  lengo la kutungwa kwa kanuni hizo ni kuweka utaratibu mzuri ambao utasaidia kuzibiti matendo ya udhalilishaji yasiongezeke katika jamii na sio kama wanavydhani wengine kuwa ni kuungilia sharia kuu za nchi.

Akihairisha semina hiyo Mratibu wa TAMWA Pemba Fat hiya Mussa Khamis amewashukuru wote kwa michango yao waliyoitoa na kusema kuwa  marekebisho yatakayofanya kutokana ya michango iliyotolewa anaamini sharia hizo zitakapo rudi katika shehia na kuanza kutumika zitaleta mafanikia makubwa katika kupambana na janga la udhalilishaji wa wanawake na watoto.

Na Othman Ali Juma - Pemba.

Comments