Wauguzi watakiwa kushirikiana katika kazi zao.

Image result for wauguzi
Wauguzi Nchini wametakiwa kufanya kazi kwamashirikiano, upendo na uadilifu huku wakizingatia maadili kwa kuwahudumia wagonjwa kkwenye wakati unaofaa.

Wametakiwa kuhakikisha wanatoa huduma zenye usalama na bora kufuatana na mabadiliko ya sanyasi na teknolojia ili kuboresha utumishi wao kwa wagonjwa na sifa kwa taifa.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Chake chake Rashid Hadidi Hamad huko ukumbi wa baraza la mji chake chake katika maadhimisho ya siku ya wauguzi na wakunga duniani.

Mkuu huyo amesema inasikitisha kuona muuguzi anamnyanyasa mgonjwa na kumkejeli jambo ambalo linavunja heshima na maadili ya kazi yake.

Mapema afisa uendeshaji tiba Wizara ya afya Pemba Dr Yussuf Hamad Idd amesema wauguzi wanawajibu wa kujitolea kwa moyo wa huruma na kuwasaidia wengine katika kuithamini kazi yao.

Katika risala yao wauguzi hao wamesema licha ya kazi ngumu waliyonayo bado wanakosa thamani na hukatishwa tamaa kwa kukosa utetezi na kuendelea kuambiwa kwamba uuguzi ni kazi ya wito.

Comments