Wananchi
kisiwani Pemba wametakiwa kulipa kodi kwa wakati nakudai risi pale wanapo nunu
bidhaa ili kuiwezesha serekali kutoa huduma bora kwa wananchi wake.
Akizungumza
na wananchi wa mji wa chake chake Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar
(ZRB) Makame Khamis mohd amesema ili serekali iweze kutekeleza wajibu wake
ipasavyo inampasa kila mwananchi kuweza kulipa kodi na kudai risiti kwa kile
watacho kinunua.
Amesema
kudai risi kutamuwezesha mteja kuwa na uhakika juu yakile anacho kinunua kuwa
kimeweza kuchangia sehemu ya mapato kwa serekali.
Amefahamisha
kuwa ili kuondoa uvujaji na ukwepaji wa mapato nilazima kila mmoja anapo uza na
kukunua kuhakikisha anakua narisiti na kuiwezesha Mamlaka hiyo kukusanya mapato
kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.
Ameeleza
kuwa mafanikio yaharaka hayawezi kupatikana endapo wananchi na wadau wa
maendeleo watakwepa kulipa kodi hiyo kila mmoja kwa nafasi yake awajibike
ipasavyo na kuleta mabadiliko kwa wananchi wote.
Aidha
ametoa wito kwa wananchi kuthamini juhudi zinazo chukuliwa na serekali za
kuwaletea maendeleo wakiamini kuwa yote yanatokana na juhudi za kodi zinazo
kusanywa Mamlaka ya Mapato Zanzibar ( ZRB ).
Comments