Upepo mkali waezua nyumba 13 Mkoani Pemba.


Image result for upepo mkali tanzaniaJUMLA  ya Nyumba kumi na tatu zimeathirika na Upepo Mkali Ulovuma majira ya saa nane za Usiku wa kuamkia jana  katika shehia ya Stahabu na Michenzani Wilaya ya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba.

Upepo huo ulozuka kijijini huko haukuwa wa hali ya kawaida kwani uliwashtua wakaazi wa maeneo hayo na kupelekea kuezuka mapaa na   nyumba  moja kuanguka .

Akitoa  pole kwa waathirika hao Mratibu wa kukabiliana na maafa kutoka Ofisi ya Makamo wa pili wa rais Pemba, Khamis Arazak Khamis, aliwataka waathirika hao kuwa wastahamilivu  kutokana na maafa waliyopata kwani hali hiyo nikutokana na mipango ya Mungu .

Aidha Mratibu huyo aliwataka  wanajamii kuchukua tahadhari katika kujikinga na maafa yanayoweza kutokea  kipindi hiki cha mvua za masika zinazoendelea kunyesha kwa kuondosha miti mikubwa iliyokaribu na nyumba zao.

"Kwa kweli wananchi wetu kwanza muwe pole kwa maafa haya  kwani mumepata hasara kubwa lakini tunakuombeni tufuate ushsuri wa watalamu wetu wa mamlaka wa hali ya hewa kuacha kujenga nyumba karibu na miti mikubwa na sehemu za mabonde yanayokaa maji".

Nae Sheha wa shehia ya Stahabu  Haji Faki Kombo ,alisema baada ya kutokea maafa hayo jambo la kwanza alitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya Mkoani ambae ndie mwenye dhamana ya Wilaya  ili kuweza kuchukua hatua kuzifikisha sehemu husika  zinazokabiliana na maafa pamoja na kupeleka majina ya waathirika.

Hata hivyo alisema kuna baadhi ya waathirika nyumba zao ziliharibika vibaya sana na kulazimika kuwahamisha ndani ya nyumba hizo na kupatiwa hifadhi ya muda kwa sasa.

Nae Aisha Abdalla Suleiman ,mkaaz wa stahabu alopatwa na maafa hayo alilazimika kuhama nyumba yake kwani ime ezuka yote  na kwa sasa haikaliki kutokana na hali hiyo.

Kwa upande wake Mtumwa Dadi Shasli miongoni mwa waathirika wa nyumba yake kuezuka mapaa nae amelazimika kuhama kwa muda.

Hata hivyo aliwashukuru wananchi kwa kushirikiana kwa pamoja na kuwapa msaada tangu kutokea tukio hilo na kuwaomba viongozi wa serikali walofika kijijini hapo kuwasaidia .

Comments