Akizungumza
katika kongamano la kuwatambua mafundi hao lililofanyika katika ukumbi wa
makonyo Chake Chake Mhandisi kutoka mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar Mkubwa
Ibrahim Khamis amesema, utaratibu huo utasaidia kuondosha tatizo la ajira kwa
vijana.
Amesema
kuwa, mafundi waliyo nje ya mfumo rasmi wa mafunzo, wanakabiliwa na changamoto
ya kutotambulika, jambo ambalo husababisha kukosa ajira, kupata malipo kidogo,
hivyo vyeti watakavyopewa baada ya mafunzo vitawasaidia kupata kazi na zenye
kipato kinacholingana na kazi zao.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar Bakar Ali
Suleiman ameeleza kuwa, lengo la kongamano hilo ni utanuzi wa mfumo wa mafunzo
ya amali kwenda mbali zaidi mpaka kuwafikia mafundi wasio na vyeti, ili nao
waweze kuhakikiwa, kutathminiwa na kutambulika.
Nae
mwakilishi wa Shirika la Kazi Ulimwenguni (ILO) Albert Okali amesema, pamoja na
kuwa mafundi hao ndio wengi katika soko la ajira Afrika na ndio wanaochangia
nafasi kubwa ya uchumi wa nchi, lakini bado kundi hilo limesahaulika kutokana
na kukosa utambulisho rasmi, ambao ndio unaoweza kumpa fursa mbali mbali katika
jamii.
Kwa
upande wa washiriki wa kongamano hilo walishukuru kupata fursa hiyo ya mafunzo
na kupatiwa vyeti na kusema kwamba itawasaidia kutambulika rasmi katika jamii
na kupata kazi kwa urahisi.
Kongamano
hilo la siku mbili limewashirikisha mafundi mbali mbali waliojifunza nje ya
mfumo rasmi wa mafunzo (wasio na vyeti), lilifanyika katika Ukumbi wa Makonyo
Chake Chake, kwa lengo la kutambulika katika jamii, ili wapate ajira na
kuondokana na maisha duni.
Comments