Mvua yakatisha safari za wananchi wa mikoa miwili Kisiwani Pemba.


Mvua yakatisha mawasiliano baina ya Mkoa wa kaskazini Pemba na Kusini Pemba baada ya daraja la chamanangwe kujaa maji na watu kushindwa kupitika.

Hii ni mara ya Pili kwa daraja hilo kujaamaji kama ilivo tokea mwaka 2017 katika mvua zamasika.

Barabara hii ni njia kuu inayotumiwa na wananchi waliowengi kisiwani Pemba katika kufuata huduma kutoka mkoa mmoja kwenda mwengine.

Wakizungumza kwa maskitiko wananchi walio kwama katika eneo la Daraja la chamanangwe Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba wamesema ipohaja kwa Serekali ya Mapinduzi Zanzibar kulishulikia daraja hilo kwani mvua zinapokua kubwa hujaamaji na kushindwa kuendelea na safari zao zakujitafutia maisha.

Aidha wameitaka Wizara ya ujenzi na Usafirishaji kuwatatulia kesro za daraja hilo kwani ndio njia pekee inayo warahisishia kufika makazini kwa muda muafaka.

Kwamujibu wa vyanzo vyetu vya habari hali hii pia imejitokeza katika daraja la Piki kadhalika katika maendeo ya Vitongoji.












Comments