
KAMATI ya siasa ya
Mkoa wa Kaskazini Pemba, imesema imefurahishwa na utekelezaji wa shughuli za
wizara ya kilimo katika kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2015-2020 katika kuwapatia
huduma wananchi wake.
Mwenyekiti wa Kamati
ya siasa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mberwa Hamad Mberwa ameseyasema hayo katika
kikao cha majumuisho ya ziara ya kukagua maeneo ya Wizara ya Kilimo kupitia
Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM ).
Mberwa amesema, kupitia Chama cha Mapinduzi kamati yao
itaendelea kutoa ushirikiano na Wizara
ya kilimo kwa kufuatilia utekelezaji katika kufikia malengo ya Ilani pamoja na
kupambana na wanaofanya uharibifu wa rasilimali za nchi kwa faida ya taifa.
Afisa Mdhamini Wizara ya Kilimo ,Maliasili, Mifugo na Uvuvi
Pemba, Sihaba Haji Vuai, amesema kwa kiasi kikubwa imekuwa ikijitahidi
kutekeleza majumu yake kwa kwa ufanisi lakini wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu
wa ushirikiano kutoka kwa baadhi ya watendaji wa serikali.
Mapema akitoa maelezo kwa kamati ya siasa, juu ya uoteshaji wa miche ya minazi huko Chamanangwe,
Afisa Mkuu Idara ya Misitu na Mali asili zisizorejesheka, Said Juma Ali, amesema
wanategemea kufanikiwa katika utekelezaji wa Programu ya kurejesha uoto wa
asili ya minazi kwa asilimia 98.
Kwa upande wao wananchi waliobahatika kukaguliwa, Miradi yao
wamesema wamefajika sana kutokana uamuzi wa Serikali kufanya ziara za kuwaona
juhudi zao pamoja na kuwasaidia kila hali itakapo ruhusu.
Comments