
Ushauri huo
umetolewa na SSP Hamad Mbarouk Rashid ,ambae ni Mratibu Mwandamizi wa
Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba , hapo Ukumbi wa Jamuhuri holi Wete wakati
alipokiwa akizindua rasmi Campuni hiyo.
Alisema
kufunguliwa kwa Campuni hiyo ndani ya Mkoa huo itaweza kusaidia
harakati za ulinzi katika Ofisi za Serikali na tasisi za watu
binafsi kwani ni muhimu sana katika jamii itakuunguza matendo ya wizi na
uhalifu .
Aidha alisema
kuwa vijana hao wanatakiwa kuwa na moyo wa kujituma na kujitolea pamoja na kuwa
na Uzalendo wa kuipenda nchi yao kwa kutoa ulinzi hata kwenye shughuli za
kitaifa.
"Mm
niwapongeze vijana haoambao kwa kukubali kujitolea kunda Campuni na Wazee
walotoa wazo hilo wamefanya jambo zuri la kupigiwa mfano sasa fanyeni
kazi vijana " alisema.
Mratibu huyo
wa polisinaliwaomba vijana hao kuwa na uwadilifu kwenye kazi na kujiepusha na
matendo ya rushwa kwani yatashusha hadhi na heshima kwenye Campuni yao na
kukosa uwaminifu.
Said Omar
Said ,ambae ni miongoni wa vijana hao wa Campuni ua Ulinzi ya Bright Security
,alisema watatenda haki kwenye kazi zao na kujiepusha na matendo ya
rushwa ambayo yatashusha nidhamu ya ulinzi.
Hata hivyo
aliwaomba wafanya biashara na tasisi za serikali kuwatumilia kwenye kazi
za Ulinzi kwani wengi wao wamepata kozi wamepata mafunzo kutoka Jeshi la
kujenga Uchumi JKU ,JKT na Mafunzo ya mgambo na kuwafanya
kujua sheria za ulinzi na mambo mengine.
Kwa upande
wake Asya Hamad Omar ,alisema kupitia Campuni hiyo Mkoa wa kaskazini Pemba
umejikomboa kwani ndio mara ya kwanza kufanyika jambo hilo.
Akitoa neno
la shukurani kwa mgeni rasmi na wageni walikwa Mzee wa kamati hiyo
Muhammed Said Muhammed ,wamelishukuru jeshi la polisi kwa kukubaliana ombi lao
la kuundwa kwa Campuny hiyo na kuwataka kuilea na kuwapa maelekezo ya kiulinzi
pamoja na kuwapatia baadhi ya vifaa ambavyo watavihitaji kwenye kazi zao.
Hata hivyo
aliwaomba wananchi wa Wete na Mkoa mzima wa Kaskazini kuiyunga mkono Campuny
hiyo ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaid.
Comments