Atafutwa na Polisi kwa Kumpa Ujauzito Shemegi yake Pemba.


Image result for kamanda hassan nasirNa Mohd Khalfan- Pemba.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba limesema linamtafuta Nd. Khamis Ali Diri anaetuhumiwa kumpa ujauzito mwananfunzi wa darasa la 6 Skuli ya Msingi Kengeja.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa huwo Hassan Nassir Ali amesema mtuhumiwa huyo baada ya kufanya tendo hilo na kukimbilia Kisiwani Unguja ambapo Jeshi la Polisi linaendelea na Msako wa kumtafuta ili kumpeleka katika vyombo vya sheria.

Kamanda Nassir amesema tayari wamesha wasiliana na Polisi wa Mkoa wa Mjini Maghribi ili kuhakikisha mtuhumiwa huyo aliempa ujauzito Shemegi yake Alie muolea dadaake baba mmoja mama mmoja anakamatwa maramoja.

Wakati huo huo Mkuu huyo wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba amesema wanaendelea na uchunguzi wa kupewa ujazito mwanamke mwenye umri wa miaka 24 ambae ni bubu na mlemavu wa akili huko kaani shehia ya kengeja.

Amefahamisha kuwa majalada ya kesi hizo yanaendelea kushughulikiwa kwa taratibu za Kipolisi.

Comments