Waziri wa Kilimo Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar,
Mh. Mmanga Mjengo Mjawiri, amewataka watendaji wa wizara yake wanaoshughulika
na uoteshaji na ugawaji wa miche kuacha kutekeleza majukumu kwa kutumia mazoea
na badala yake kusimamia na kufatilia uoteshwaji wa miche inayotolewa kufikia
lengo la serikali.
Mh.
Mmanga ameyasema hayo kwa nyakati tofauti wakati alipofanya ziara fupi
yakutembelea nasari za kuotesha miche ya mikarafuu huko mkata maini na
chanjaani wilaya ya chake chake.
Amesema,
iwapo maafisa watasimamia vyema katika malezi ya miche itakayotolewa itasaidia
miche kustawi zaidi kwa kuisaidia serikali kuweza kutimiza malengo yake ya
kunyanyua wananchi.
Kwa
upande wao, wafanyakazi wa nasari za miche ya mikarafuu wameahidi kusimamia
vyema taratibu zinazohitajika ili kukamilisha malengo yalio kusudiwa.
Aidha
wameiomba serikali kupitia wizara husika kuwatatulia changamoto ya upatikanaji
wa maji na kuongezewa wafanyakazi , katika kuimarisha ongezeko la miche ambayo
ndio kilio cha wananchi.
Comments