Samakai aina ya Chongowe onekana Kinowe Pemba.

Image may contain: one or more people, outdoor, water and nature
Samaki mkubwa mwenye urefu wa zaidi ya mita kumi na tano, upana mita saba anaejulikana kwa jina maarufu chongowe ameonekana  katika bahari ya kinowe , wilaya ya micheweni, mkoa wa kaskazini pemba ambapo wananchi wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya samaki huyo ili kunusuru kutokea madhara.

Akizungumza na wananchi huko katika bandari ya kinowe wilaya ya micheweni kaimu afisa mkuu wa idara ya maendeleo ya uvuvi Hidaya Khamis Hamad, amewaasa wananchi kutomtumia samaki huyo kwa matumizi ya kula, ili kunusuru afya zao.

Kwa upande wake, afisa uvuvi pemba , aAli Rashid Hamad, amesema idara ya maendeleo ya uvuvi kwa kushirikiana na taasisi nyengine watafanya uchunguzi  ili waweze kutambua aina  ya samaki  kwa faida ya   jamii na taifa kwa ujumla.

Nae   sheha wa shehia ya kinowe Juma Adi Haji amesisitiza juu ya matumizi sahihi ya  mafuta ya samaki huyo ,ili waweze kuwa salama.

Kwa upande wao wananchi waliofika katika eneo hilo kwa ajili ya kuchukua mafuta akiwemo Asaa Hamad Ali  amesema watatumia mafuta hayo kwa ajili ya tiba na si vyenginevyo kwa kufuata maelekezo na ushauri wa serikali.

Comments