Wauza chunvi wapewa somo kuboresha biashara yao.

Image result for chunvi
Wazalishaji wa Chunvi wa eneo la Shengejuu Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba wametakiwa  kuhakikisha Chunvi wanayo zalisha wanaitia madini joto  kabala ya kumuzia mfanya biashara na kumfikia mtumiaji   ili iwe salama kwa afya za watumiaji huko majumbani kwao .

Ili kuweza kuepuka madhara yatokanayo na utumiaji wa chunvi ilokosa madini joto ni jukumu la kila mzalishaji wa chunvi kutia madini joto mara tu baada ya kukausha kabla ya kuipeleka kiwandani ama  kuipeki kwenye mifuko maalumu ya kuhifadhia.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa kitengo cha lishe Pemba Raya Mkoko Hassan  wakati alipokuwa akitoa mafunzo kwa wazalishaji chunvi huko Shengejuu  eno la Ambasha Wilaya ya wete.

Alisema kutokana na tamko la serikal kwamba madhara yatokanayo upungufu wa madini joto ni tatizo kubwa kwa Tanzania ambapo asilimia 35 ya wanawake walio kwenye umri wa kuzaa wako kwenye hatari ya kuzaa watoto wenye mtindio wa ubongo na kupata ulemavu wa kudumunwa viuongo mbali mbali mwilini.

Mkuu huyo wa kitengo alisema ili kumaliza kwa tatizo hilo ni kutumia chunvi yenye madini joto  kila siku .

“Wazalishaji wa chunvi munatakiwa kuwa na uwaminifu kwenye kazi ya uzalishaji wa chunvi tieni madini joto kwani baadhi ya chunvi hazina”.alisema  Mkuu huyo.

Akitaja sheria Chini ya Mamlaka ya Chakula na Dawa ya mwaka 2003 sura 219,ya kanuni namba 122(1)(c) ya mwaka 2010 imeweka kwa wazalishaji na wauzaji wa chunvi kuzalisha na kuingiza chunvi yenye madini joto.

Akizungumzia njia ya uchangaji wa chunvi na madini joto alisema  mtu anatakiwa kutayarisha rundo la tani 3 ya chunvi safi ya mawe iliyokauka ni sawa na mifuko 60 ya kilo 50 au tani sita za chunvi laini ambayo ni sawa na mifuko 120 ya kilo 50.

Hata hivyo aliwataka wazalishaji hao hao kupima gramu 240 za maduni joto na kuchanganya kwenye lita 20 za maji barid yasiyokuwa na chumvi kwenye ndoo hapo itakuwa salama chunvi hiyo .

“Jitahidini kufata maelekezo tuanayokupeni wazalishaji chunvi ili kuepuka madhara kwa watumiaji pamoja na kufungiwa nyie wazalishaji”. alisema.

Nae Asaa Ali Hamad, mzalishaji wa chunvi huko Shenge juu eno la Ambasha alisema baada ya kupat Elimu hiyo ya kitalamu wataweza kufanya biashara zao kwa uhakika  zaid.

Alifahamisha kwamba iwapo mkulima wa chunvi ataweza kufata taratibu wanazopatiwa na watalamu wao wanatapiga hatua kimaebdeleo.

Akizungumzia mafankio alopata tangu kuanza kwa kazi hiyo ameweza kujenga nyumba ya makaazi na kuishi bila ya kumtegemea mtu na kuweza kuajiri wafanyakazi wa kuzalisha chunvi huko kwwnye mabwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kanda anae simamia shughuli za uzalishaji chunvi huko Shengejuu zoni (A)  Hamad Omae Salum , alisema eneo lake lina Viwanda 22 vya uzalishaji Chunvi vilivyo sajiliwa    na mamlaka husika.

Akitaja ugumu wa kazi hiyo kwa baadhi ya wakati nipale wakulima wake wanapo hitaji madini joto kutopata kwa wakati  kutoka na masafa ya maeneo  yao kuwapata kwa urahisi.Image result for chunvi

Comments