Wakuu wa idara Pemba watakiwa kuandaa Ripoti zao za kazi.


Image result for pemba
Afisa Mdhamini wa Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi  wa Umma na Utawala Bora  Pemba  Massoud Ali Muhammed, amewataka Wakuu wa maidara na taa sisi  zilonje ya Wizara yake  kuandaa ripoti ya kazi ya Utekelezaji wa kazi kwa kipindi cha mwaka 2017 na 2018 kuanzia mwez  wa nane hadi Disemba  ambazo wamezifanya kwa kutekeleza ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu ya Mwaka 2015 hadi 2020  .

Uwandaaji wa ripoti hizo kwa  kipindi cha miaka miwili zita somwa katika majumuoisho baada ya kumaliza ziara ya rais wa Zanzibar Dk Ali Muhammed Shein ,  ambaye anatarajiwa  kufanya ziara hiyo wiki inayofatia  kisiwani Pemba.

Kauli hiyo ameitoa huko ofisni kwake wakati alipokuwa akizungumza na Wakuu na Maidara na baadhi ya taasisi zilizo njee  ya Wizara yake ambazo zina jitegemea .

Alisema taarifa hizo zitaweza kueleza utkelezaji wa kazi zao ambazo zimefanywa      na idara ama taasisi ambazo zimezwa kuyatekeleza kwa misingi ya  ilani ya Uchaguzi kama ilivyo ahidi kuwafanyia maendeleo wananchi wake  kama walivyo ahid wakati wa kambeni za uchaguzi  kwamba wataitumia ilani hiyo kwa kulete  huduma nchini.

Viongozi wakati  wa Uchaguzi waliahidi kuwatumikia wananchi wake  huduma za maendeleo  zilobora kwa ilani hiyo .

“ Wakuu wa maidara  pitieni kifungu kimoja baada ya kimoja na utekelezaji  ambapo itaweza kufahamika na pale penye mspungufunkuganyiwa marekebisho mapema”. alisema Mdhamuni huyo.

Aidha alisema kuwa Utekelezaji wa ilani ya CCM ya  Uchaguzi sio kufanya siasa kwani ndio inayowaongoza kufanya shughuli za maendeleo  ikiwemo  Mkuuza na mambo mengine ya maendeleo kwa lengo la kuwatumikia wananchi.

“Ilani ya Uchaguzi ndio mkataba wao ulowafunga kutekeleza kwa vitendo na hili sio la Wizara moja tu ni kila Wizara inatakiwa kufuta kwa  katiba ,sheria ,utumishi wa Umma na Utawa bora bila ya kuathiri mipango kazi yenu” .alifahamisha.

Hata hivyo Mdhamini huyo alisema kuwa wakuu wa idara na taasisi za serikali wasione tabu kuiyelezea ilani ya Uchaguzi na kuitumikia kwenye mipango kazi yao.

Aliwahimiza wakuu wa maidara hao siku ya Uwasilishwaji wa ripoti ya Utekeleza  wa kazi zilizofanywa kuwepo siku hiyo ili kuweza kuichangia pale patakapokuwa na mapungufu .

Kwa Upande wake afisa Mdhamini wa tume ya maadili Pemba Hanuna Ibrahim Massoud, alisema  uandaji wa ripoti hizo ni muhimu kutayarishwa mapema ili kuweza kupitiwa na kuangaliwa ikiwa kuna mapungufu kufanyiwa marekebisho  kwa wakati.

Hata hivyo alifahsmisha  kuwa uwandaaji wa ripoti hizo  sio wa mtu mmoja unahitaji kushirikiana kwa pamoja ili kuweza  kuyaelezea yale yalotekelezwa  ndani ya ilani  ya Uchaguzi  CCM ya Mwaka 2015 /2020 .

Hata hivyo Mdhamini huyo aliwaomba wakuu hao wa maidara kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu katika wizara yake anayoifanyia kazi kwa sasa.

Kwa upande wake Mdhamini wa ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa hesabu za Serikali Said Khamis Juma ,alisema ili kufanya vyema majukumu ya kazi zao ni kuitekeleza ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu  ambayo ndio katiba  ya shughuli za maendeleo na mipango ya nchi.

Hata hivyo aliwaomba wakuu wamaidara waloshiriki mkutano huo kumpa ushirikiano wa kazi zake ndani ya ofisi kwani ameshika nafasi hiyo baada ya mabadiliko yalofanyika hivi karibuni .

Wakuu wa maidara  alizozungumza nazo ni  Tume ya Maadili, Mahkama ,Chuo cha Utumi wa Umma Ipa Pemba , Mamlaka ya kuzuia rushwa ,Ofisi ya Mufti na Ofisi Mdhibit Mkuu wa hesabu za serikali Pemba .

Comments