Shehia tatu za Wilaya ya micheweni zapewa mafunzo.


Related image
Wananchi wa Wilaya ya Micheweni wameshauriwa kuwa na tahadhari juu ya utendaji wa shughuli zao za kimaendeleo kwa kuhakikisha  wanaweka miundombinu itakayosaidia uokozi pindi maafa yanapotokea.

Mkuu wa wilaya ya Micheweni Salama Mbarouk Khatib ametoa ushauri huo katika mafunzo juu ya uwelewa wa kukabiliana na maafa kwa wananchi wa  Micheweni yaliyoendeshwa na kamisheni ya kukabiliana na maafa Kisiwani Pemba .

Mkuu huyo  amesema jamii inawajibu wa kufuata taratibu za ujenzi uliosalama na kuweka usafi wa  mazingira ili kuwa rahisi kujikinga na majanga hayo .

Awali Kaimu mratibu wa kamisheni ya kukabiliana na maafa Pemba Mbela Issa Mbela amesema wilaya ya micheweni imekuwa na uzoefu wa kutokea maafa kutokana na mazingira yake kukabiliwa na ukame wa mara kwa mara.

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema licha ya kuwepo elimu za mara kwa mara bado kuna maeneo hasa ya visiwa vidogo vidogo yameanza kuleta ishara ya kutokea maafa na tahadhari inapaswa kuchukuliwa .

Shehia zilizopatiwa mafunzo hayo ni pamoja na Msuka magharibi, Tumbe magharibi na  Shumba mjini .

Comments