Waziri wa Elimu Zanzibar afungua kituo cha afya kiuyu kipangani Pemba.

Image may contain: 2 people, people sittingWAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma amesema malengo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ya kujenga vituo vya afya mijini na vijijini ni kuwapatia wananchi wake huduma bora za kiafya.

Akizungumza baada ya kufungua kituo kipya cha afya cha Kiuyu Kipangani kiliopo Wilaya ya Micheweni Pemba, ikiwa ni shamra shanra za maadhimisho ya miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe Riziki amesema Serikali ipo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi katika kutoa huduma mbalimbali ikiwemi afya kama ilivyoahidi katika ilani yake, hivyo ni lazima kuthamini juhudi hizo.

Amewataka waanchi kukitumia kituo hicho katika kupata huduma mbalimbali za afya hasa kina mama kwa kujifungulia ndani ya kituo hicho badala ya kujifungulia majumbani, ili linapotokea tatizo liweze kutatuliwa kwa haraka na kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto.

Aidha amewataka akina baba kuwasimamia akina mama juu ya suala hilo la kutojifungulia majumbani pamoja na kuwaunga mkono wakati wanapokwenda kliniki ili kujua matatizo waliyonayo na kuwasaidia.

Aidha amewataka wataalamu wa afya kuendelea kutoa huduma bora kwa wagonjwa wao na kutowanyanyapaa, kwani kazi hiyo ni ngumu na inahitaji upendo na pia kuacha tabia ya kuwachangisha wananchi kwani huduma za matibabu ya afya ni bure.

Pia amewataka kuvitunza vifaa tiba ili viweze kutumika kwa muda mrefu kwani vina gharama kubwa, na kuwatahadharisha wenye tabia ya kuviuza vifaa hivyo au dawa na ataebainika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Hata hivyo amewashukuru washirika wa maendeleo Serikali ya Uholanzi chini ya kitengo chake cha ORIO pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa juhudi walizochukua kwa kujenga kituo hicho katika hali ya ubora zaidi pamoja na kuweka vifaa vya kisasa.

Akisoma taarifa juu ya ujenzi wa kituo hicho cha afya, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya bi Halima Maulid Salum amesema ujenzi wa kituo hicho ni miongoni mwa vituo 15 vilivyojengwa kwa unguja na Pemba, ambapo ni miongoni mwa matunda ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar.Image may contain: 2 people, people standingImage may contain: 2 people, people smiling, people standingImage may contain: 5 people, closeup and outdoorImage may contain: 21 people, people smiling, crowdImage may contain: 5 people, people smiling, crowd and outdoor

Comments