
Akizungunza wakati alipomkaribisha rais wa Zanzibar kuzungumza na
wananchi baada ya kufungua Skuli ya Msingi Chimba, iliyopo Wilaya ya
Micheweni, ikiwa ni shamra shamra za Sherehe za kutimiza miaka 55 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe Riziki amesema walitakiwa kufanya hivyo bila ya kujali itikadi za kisiasa au kitu chochote.
Amesema kuna mafanikio makubwa yamepatikana katika uongozi wa Dr. Shein
ambapo amewataka wananchi kuunga mkono juhudi hizo ili kupata maendeleo
zaidi.
Amesema lengo la kujenga madarasa hayo ni kuwapunguzia watoto kufata elimu masafa ya mbali pamoja na kuwafanya kupata elimu bora.
Skuli ya msingi Chimba imejengwa na serikali ya mapinduzi ya zanzibar kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha chimba, mfuko wa jimbo wa Mwakilishi na Mbunge pamoja na Halmashauri na ina madarasa manne na ofisi za walimu mbili.
Amesema lengo la kujenga madarasa hayo ni kuwapunguzia watoto kufata elimu masafa ya mbali pamoja na kuwafanya kupata elimu bora.
Skuli ya msingi Chimba imejengwa na serikali ya mapinduzi ya zanzibar kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha chimba, mfuko wa jimbo wa Mwakilishi na Mbunge pamoja na Halmashauri na ina madarasa manne na ofisi za walimu mbili.

Comments