
Wamiliki
wa vituo vya mafuta Kisiwani Pemba
wametakiwa kuwa na mpango maalum wa kujiwekea miundombinu bora ya usalama kwenye sehemu zao ili kuwa
rahisi kujiokoa pindi kunapotokea maafa .
Wameshauriwa
kuwapa mafunzo wafanyakazi wao pamoja na kutenga vifaa vya huduma ya kwanza ili
kuwa na uwezo wa kujisaidia wenyewe kabla ya kutokea athari zaidi .
Hayo
yamesemwa kwa nyakati tofauti na Mkuu wa Operation ya kukabiliana na maafa Zanzibar
Shaaban Hassan Ramadhan katika ziara ya ukaguzi wa bohari na vituo vya mafuta
kisiwani humo.
Amesema
katika ukaguzi huo wamegundua mapungufu mengi ya kiusalama huku akitoa agizo la
miezi mitatu kwa wamiliki kuyafanyia kazi mapungu hayo kabla ya kutokea maafa
yasiyotarajiwa .
Katika
ziara hiyo mkuu wa operation ya uokozi kutoka kikosi cha zimamoto ali abdi
hashim amesema baadhi ya vituo havina dawa mitungi ya kisasa ya kuzimia moto
wala matangi ya maji hivyo kuwa vigumu kwao kuweza kujiokoa .
Nao
baadhi ya wasimamizi wa vituo hivyo vya mafuta wamesema watayafanyia kazi
mapungufu madogo madogo yaliopo na yale makubwa watawasiliana na wamiliki wao
kwa ajili ya hatua .
Comments