Tamwa kumaliza matatizo yalioibuliwa na Paza.


Tamwa imeomba kuendeleza mradi wa PAZA ili matatizo yalio ibuliwa yamalizike.

Hayo yameelezwa na Bi Salma  Ali Hamadi miaka (50) kufatia kuepo kwa tatizo la ujenzi wa uzio katika skuli ya Muungoni ambalo halijatekelezwa wananchi wa muungoni wameshindwa kujua sababu ya kutojengwa kwa ujenzi wa uzio huo .

Amesema Mradi wa PAZA umewawezesha wananchi wa Muungoni kuhamasika na kuweza kufuatilia njia za kutatua matatizo mengi ikiwemo tatizo la uchakavu jengo la afya ambapo limeboreshwa  na huduma zinapatikana ipasavyo hospitalini hapo.

Wakizungumzia huduma  ya maji safi na salama  wakaazi wa shehia ya Muungoni wilaya ya Kusini  Unguja wamesema huduma hio imepatikana baada ya kupata mashine mpya ya kuvutia maji katika kisima kutokana na kuhamasika na Mradi wa kukuza uwajibikaji Zanzibar (PAZA) unaosimamiwa na chama cha waandishi wahabari wanawake Zanzibar(TAMWA-ZANZIBAR).

Aidha amesema mradi huo umesaidia kuwaletea visima vya maji safi na salama  ingiwa maji hayo yanachumvi kidogo lakini umeweza kuwaondolea tatizo sugu la maji kutokana na huduma hiyo kuwa muhimu katika jamii.
.
Sambamba na hayo amewashukuru watendaji kazi wa ofisi ya Halmashauri za wilaya kwa namna walivyowajibika katika kutekeleza majukumu yao kwa wakati na wananchi wameridhirika kwani tatizo la maji lilikua kubwa.

Kwa upande wa Asasi za kiraia na matandao wa Ardhi wilaya ya kusini, Halda Nassor Haji ambae anawahamasisha waakazi wa shehia ya Kitogani na Muungoni amesema watendaji wa Halmashauri wameshafanya tathmini ya ujenzi wa uzio katika skuli hiyo lakini bado halijatiwa katika utaratibu  wa mpango wa matumizi ya kifedha(bajeti) .

Hivyo amewaomba wananchi waendelee kuwa wavumilivu na endapo ujenzi wa uzio, huo utakapokua tayari watapewa taarifa .

NA RAHMA MOH’D.

Comments