
Afisa Afya wa wilaya ya kusini Jaku Ameir Issa
amesema ofisi yao inaendelea kusimamia huduma za afya ili kuhakikisha wanawake
wa mkoa huo wanapata huduma za Afya ya Uzazi bure kwa kupatikana madaktari wakutosha katika wila hiyo.
Ameyasema hayo kupitia Mradi
wa kukuza Uwajibikaji Zanzibar (PAZA) unaosimamiwa na Chama Cha wa Waandishi wa
Habari wanawake Zanzibar (TAMWA- ZANZIBAR). Amesema wakaazi wa kijiji cha
Kitogani wamehamasiki kuibua matatizo mbalimbali kupitia mkutano mkuu wa kijiji
ambao uliwashirikisha wananchi wa kijiji cha Kitogani kwa lengo la kuibua changamoto zinazo
wakabili kijijini hapo.
Akifafanua miongoni mwa
changamoto zilizokuwa zikiwakabili
ambazo zimetatuliwa kupitia mradi
wa (PAZA) kwa kuboreshwa hospitali ya Kitogani ambapo jengo la hospital
hiyo lilikua limechakaa sana pamoja ukosefu wa madaktari.
Hata hiovyo amesema jumla wa watu wenye ulemavu 33,
wanawake 42 na vijana 18 walifika ofisini kwake kupeleka maombi ya malalamiko
ya kuomba kuboreshwa huduma ya afya.
Akizungumza
kwa niaba ya wanakijiji wa kitogani Bi Khadija Kheiri mwenye umri wa miaka (58) amesema
PAZA imetusaidia kupata huduma ya maji
safi na salama , jengo la hospitali limejengwa vizuri ingawa hatujakabidhiwa
lakini limeshafanyiwa ukarabati mzuri limependeza.
Khadija amesema wananchi wa
Kijiji cha kitogani walikuwa wamekabiliwa na matatizo mengi ikiwemo la maji
safi na salama, ukosefu wa walimu, huduma ya afya pia ilikuwa mbovu.
Sambamba na hayo ameeleza
kuwa Mradi wa PAZA umesaidia
kuwaelimisha wananchi taratibu za kufuatilia ufumbuzi wa
matatizo katika Ofisi ya Halmashauri za wilaya na kuwajua maafisa wa
serikali kawaajili ya kuwajibisha katika majukumu yao.
Bi Khadija amesema wananchi wa Kijiji cha kitogani
walikuwa wamekabiliwa na matatizo mengi ikiwemo la maji safi na salama, ukosefu
wa walimu, huduma ya afya pia ilikuwa mbovu.
Mradi wa kukuza Uwajibikaji
Zanzibar (PAZA) ulianza mwaka jana kwa lengo la kukuza Uwajibikaji Zanzibar ili
kuwahamasisha wananchi njia za kutatua matizo yanayozunguuka katika jamii na
utarajiwa kumalizika mwakani
.
Na RAHMA MOH’D
Comments