Wakaazi wa Kitogani wameomba watendaji wa Mradi wa PAZA
kuendeleea na mradi kutokana na bado
watu wanamuamko mdogo wa kuhudhuri mkutano wa kijiji kutokana na itikadi za
kisiasa .
Akizungumza na muandihi wa
habari hizi Amesema baadhi ya watu wanapoitwa kuhudhuria kwenye kikao cha
kijiji wanapuunza na kuendelea na shughuli zao na hatimae kukosa taarifa za
maendeleokatika maeneo yao .
Kwa upande wa wanufaika wa
Mradi huo Wahida Khatib Ali mika (24) mkaazi wa Muungoni amesema kupitia mradi
wa PAZA wanaelimika njia ya kuwafuata watendaji wa Halmashauri na kujua
majukumu yao.
Hivyo ameeleza kuwa ameridhishwa utendaji wa Mradi wa PAZA kwa
umewaondolea matatizo mengi, wilaya ya kusini ikiwemo tatizo la utoro kwa
wanafunzi, shida ya mji safi na salama, ukarabati wa vitua vya afya na majengo
ya skuli.
Amesema Wahida “ Paza imenielimsha naweza kuandika
barua ya malalamiko ya shida ya maji na kupeleka Halmashauri na kufuatilia hadi
kufikia hatua ya mafanikio, tulihudhuria mkutano sisi wote tunaweza kutatua
matatizo yetu kwa sasa”
Nae Mwana asasi za kiraia
Halda Nassor Haji miaka (32)
amesema amewashajihisha wanawake
100 elimu ya kukuza uwajibishaji katika shehia hizo ili waondokane matatizo
katika vijijini mwao .
Amesema wametumia njia ya
mkutano kuwaeleza elimu hiyo akinamama ambapo pia kila mwanakijiji alipata
fursa ya kuibua matatizo yalimkabili katika eneo lake.
Ameeleza kuwa wanaasasi wote walipewa mafuzo na chama cha
waandishi wa habari wanawake Zanzibar (TAMWA-Zanzibar) kupitia Mradi wa Kukuza
uwajibikaji Zanzibar (PAZA) na kuwataka elimu hiyo kuwafikishia wanawake wenzao
vijijini.
Jumla wa wanawake 100 wa
shehia ya Muunguno, Kitogani na Bwejuu wilaya ya kusini Unguja wamehamasikia na
elimu ya kukuza Ujibikaji Zanzibar kupitia asasi za kirai na mitandao ya
ardhi ambapo elimu hiyo imewaleta maendeleo katika maakazi yao ikiwemo
kuondokewa na tatizo la maji, afya na elimu.
NA RAHMA MOH’D
Comments