Waziri Pembe atoa neno kwa Uongozi wa Chuo Kikuu Zanzibar.

Picha ya Wizara ya Elimu ZanzibarWAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe, Riziki Pembe Juma ameutaka uongozi wa chuo kikuu cha Zanzibar (ZU) kutumia lugha ya kiswahili katika mahafali zao ili kuwawezesha washiriki kufahamu kilichokusudiwa katika mahafali hiyo.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha Makamo wa pili wa Rais Mhe. Balozi Seif Ali Iddi kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr Ali Muhammed Shein, katika Mahafali ya 16 ya Chuo hicho kibele Mkoa wa Kusini Unguja, Mh Riziki amesema hali hiyo pia itasaidia kukikuza kiswahili na kuzidi kutambulikana kimataifa.

Aidha Mhe, Riziki amewapongeza wanafunzi waliohitimu masomo yao pamoja na chuo hicho kwa kutoa nafasi za masomo ya Elimu ya juu kwa wingi, (scholarship), huku akiwataka kuongeza idadi kubwa zaidi ya nafasi hizo ili wanafunzi waweze kujiendeleza na kupata idadi kubwa ya wataalamu hapa nchini.
 Picha ya Wizara ya Elimu Zanzibar

Comments