Wanamgambo wa Daesh wafurushwa kusini magharibi mwa Libya.

Wanamgambo wa Daesh wafurushwa kusini magharibi mwa LibyaVikosi vya ulinzi vya Libya vimewafurusha mamluki wa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh katika mji wa Tazirbu wa kusini magharibi mwa nchi hiyo. 

Kamandi ya kijeshi katika eneo la Kufra huko Libya jana ilitangaza kuwa wanajeshi wa Libya wamefanikiwa kulidhibiti kikamilifu eneo la kusini magharibi mwa nchi hiyo baada ya kuwafurusha magaidi hao wa Daesh. 

Kamandi hiyo ya kijeshi ya eneo la Kufra imeongeza kuwa kundi la Daesh halina tena fursa ya kukariri mashambulizi yake dhidi ya vijiji na vitongoji vinavyolindwa na jeshi la Libya. 

Mamluki wa kundi la kigaidi la Daesh hivi karibuni walikabiliana na polisi wa Libya baada ya kufanya shambulio katika kituo kimoja cha polisi kwenye mji wa Tazirbu wa kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Katika mapigano hayo watu tisa wakiwemo polisi watano waliuawa na kumi kujeruhiwa. Siku mbili zilizopita pia, magaidi wa Daesh walionyesha picha wakidai kuwa wamewateka nyara karibu watu 20 katika shambulio walilolifanya katika kituo hicho cha polisi.

Magaidi wa kundi la Daesh wamekuwa wakifanya mashambulizi mengi katika miji ya kusini mwa Libya tangu walipoanza kutorokea katika maeneo ya msituni nchini humo baada ya kufurushwa katika mji wa bandari wa Sirte. 

parstoday

Comments