Kamisheni
inayohusika na kuwakusanya waasi hao imesema kuwa waasi hao waliorejea
nyumbani wote wamekusanywa katika kituo cha Mutobo ambapo watapatiwa
mafunzo ya kiraia kabla ya kuunganishwa na jamii zao za asili.
Baadhi
ya wanamgambo hao wa zamani waliozungumza na gazeti la Teh New Times la
nchini Rwanda wamesema kwamba, walikuwa wanahofia usalama wao nchini
Rwanda kwa sababu walipatiwa taarifa za uongo na makamanda wao na watu
wengine ambao wamekuwa na maslahi na kunufaika na kuendelea kuwepo kwa
kundi hilo la waasi.
Itakumbukwa
kuwa kwa miaka kadhaa sasa Rwanda imekuwa ikiendesha zoezi la
kuwaunganisha na familia zao waasi hao na hadi hivi sasa
imeshawaunganisha na familia hizo zaidi ya waasi wa zamani elfu kumi
huku kila muasi akipatiwa mtaji wa kuanzia maisha wa faranga za Rwanda
elfu sitini sambamba na kupatiwa mafunzo ya ujuzi wa maisha kwa ajili ya
kuanza maisha mapya uraia.
parstoday.
Comments