Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Takwimu za Bei Ofisi ya
Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Khamis Abdul-rahman Msham, alipokuwa
akizungumza na waandishi wa habari jana.
Alisema, kiwango cha mfumko wa bei cha vyakula na vinywaji visivyo na
vilevi kiliongezeka hadi asilimia 3.4 mnamo Novemba 2018 kutoka
asilimia 2.6 mwezi Oktoba 2018.
Aidha, alisema, faharisi za bei ziliongezeka hadi 108.0 mnamo Novemba 2018 ikilinganishwa na 103.4 zilizoripotiwa Novemba 2017.
Alisema, kiwango cha mfumko wa bei wa mwaka kwa vyakula kiliongezeka
hadi asilimia 3.5 kwa mwaka ulioishia Novemba 2018, ikilinganishwa na
asilimia 2.7 kwa mwaka ulioishia Oktoba, 2018.
Mkuu huyo, alisema, faharisi za bei za vyakula ziliongezeka hadi
105.0 mnamo Novemba 2018 ikilinganishwa na 101.5 iliyoripotiwa Novemba
2017.
Vilevile kiwango cha mfumko wa bei wa mwaka kwa bidhaa zisikuwa za
vyakula kiliongezeka kwa asilimia 5.2 mwezi Novemba 2018 ikilinganishwa
na asilimia 4.5 mwezi Oktoba 2018, huku faharisi za bei zikiongezeka
hadi 110.3 mwezi huo wa Novemba, ikilinganishwa na 104.9 kwa mwezi
Novemba 2017.
Bidhaa zilizochangia kuongezeka kwa mfumko wa mwaka zilikuwa ni
mchele wa mapembe (21.4%), samaki (2.5%), saruji (2.9%), mafuta ya taa
(21.2%), petrol (13.5%) na diseli (9.1%).
Kwa upande wa mfumko wa mwezi Novemba 2018, kiwango kilipungua kwa
asilimia 0.3 asilimia ikilinganishwa na asilimia 0.4 mwezi Oktoba 2018.
Pia mfumko kwa bei wa mwezi kwa vyakula na bidhaa zisizo na vilevi
mwezi ulioishia Novemba 2018, ulipungua wa asilimia hasi 1.5
ikilinganishwa na asilimia 0.9 kwa mwezi Oktoba 2018.
Alisema, kushuka kwa kasi ya mfumko wa mwezi kulichangiwa na bidhaa
kama vile mchele wa Mbeya (2.4%), Sembe (5.5%), samaki (5.8%), ndizi za
mkono mmoja (10.3%) na sukari (0.2%).
Mkuu wa Takwimu za Kiuchumi Ofisi ya Mtakwimu Mkuu, Abdulrauf
Ramadhan Abeid, alisema, kwa ujumla katika nchi tatu za Afrika Mashariki
mfumko bado unaendelea kubakia chini ya tarakimu moja na hivyo kwenda
vizuri kiuchumi.
Alisema, mfumko wa bei wa Kenya ulifikia alimia 5.58 mwezi Novemba kutoka 5.53 mwezi Oktoba wakati Uganda upo asilimia 3.0.
Mhadhiri na Mkuu wa Idara ya Uchumiya Chuo Kikuu cha Taifa cha
Zanzibar (SUZA), Dk. Suleiman Simai Msaraka, alisema, kiuchumi bado kasi
ya mfumko inaendelea vizuri na haijaathiri kimaisha, ikizingatiwa
bidhaa zilizoongezeka bei zinatoka nje na nchi kutokuwa na uwezo wa
kuzuia bei kulinganisha na soko la kimataifa.
Zanzibarleo.
Comments