ZAECA yashtukia harufu ya rushwa.

AFISA Habari wa Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) Mwanaidi Suleiman,amesema bado hakujawa na mwamko mkubwa kwa wanamichezo kutoa taarifa za rushwa wanazozishuhudia katika harakati zao za michezo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi alisema kuwa kesi  za rushwa  zipo na zinazohusiana na michezo Zanzibar, lakini kutokana na michezo inavyo chezwa jamii bado haijawa na mwamko wa kuzitolea taarifa.

Alisema kuwa hii inatokana na kwamba wanamichezo hao  walikuwa hawajui kwamba rushwa inahusika pia katika michezo  na kuamini  na inaingia katika kuhujumu uchumi.

Hata hivyo alisema kuwa mpaka sasa wanazo kesi chache zinazohusiana na rushwa michezoni ambazo wanaendelea kuzifanyia kazi.

Samabamba na hilo alisema kuwa baada ya kuona hivyo waliamua kufanya mafunzo ya  kuwaelimisha kwa kuandaa mkutano maalumu na kuwashirikisha wanamichezo  wakiwemo viongozi, waamuzi na wote wanaohusiana na michezo.

Hivyo alisema kuwa mafunzo hayo yameweza kutoa mwamko  na kujua kwamba na wao wana haki au uwezo wa kutambuwa kwamba hichi kinachofanyika katika michezo ni rushwa na wanaweza kukiripoti.

Hata hivyo alisema kuwa  mamlaka hiyo imekuwa ikizidi  kuwashajiisha na kushukuru kushirikishwa katika mambo mbali mbali wanayofanya katika kuimarisha michezo .

Zanzibarleo.

Comments