Watendaji wa Afya chake chake watakiwa kutenda vyema kwa wagonjwa.


Image result for hospitali ya chake chakeWauguzi na Wakunga wa hospitali ya Chake Chake wametakiwa kufanya kazi kwa mashirikiano na kufuata sheria kanuni za utumishi  kwa mujibu wa baraza la Wauguzi zinavyowaelekeza  majukumu yao  katika kuhudumia wagonjwa.


Baraza la Wauguzi lina sheria zake kwa wafanya kazi wake kwanza kuitumikia dhamana alopewa na kuithamini kazi yake  wakat wa kutoa huduma kwa wagonjwa wao kwani wanaonekana ndio masuli wa kila jambo linalotokea kulifahamu .


Kauli hiyo imetolewa na msaidiz Mrajis wa baraza la Wauguzi Pemba Sabra Salum Suleiman ,wakati alipokuwa akizungumza na Wauguzi na Wakunga hapo hospitali ya Chake chake katika kukumbusha  umuhimu  wa utendaji kazi wao kwani ni watu muhimu kwa jamii kutokana na kazi zao.


Alifahamisha kwamba asilimia 50 ya wafanyakazi ni Wauguzi hivyo wanatakiwa kujitambua na kuwa na madili mazuri na kutumia lugha nzuri na upole wakati wanapotoa huduma kwa wagonjwa walolazwa na wanaokwenda na kurudi.


“Nakuombeni wafanya kazi wezangu fanyeni kazi kwa kuguata sheria ya mabaraza ya Uuguzi unavyoelekeza na mtu kujua majukumu yake niyepi”.alisema Msaidizi Mrajisi huyo.


Alifahamisha kuwa mfanya kazi yoyote anatakiwa kufanya kazi kwa wakati uliopangwa ambao ni saa moja na robo wanatakiwa kukabidhiana ofisi na kwa maandishi kutoka kwa mtu wazamu alokuwepo kazini usiku.


Aidha alisema kwa watu wanaoingia kazini mchana wanatakiwa kufika kazini saa saba na nusu ili kuweza kukabidhiana zamu zao na kumkabidhi wagonjwa ambao wanahudumiwa na kupita Wodi moja moja kuwaona wagonjwa ambao wamelazwa ili iwe rahis kupatiwa matibabu.


Kwa upande  wake Afisa Muguzi  Msaidiz Pemba Dr  Omar Juma Ali ,alisema baraza la Wauguzi kupitia Sheria namba 5 ya mwaka 2014 ambayo imepitishwa na baraza la Wawakilishi imeleza mambo mengi  ikiwemo uwajibikaji wa kufanya kazi kwa uwadilifu pamoja na makosa na adhabu zake iwapo atatenda kinyume na kanuni za utumishi.


Hata hivyo aliwaomba wauguz hao na wakunga kuweka utaratibu wa kufanya vikao kila miezi mitatu kujadili changamoto za kiutendaji  ili kuweza kuzitatua kwa uwongozi wa chini kabla ya kufika uwongozi wa juu.


“Utaratibu wa kazi unahimiza kwamba kila miezi mitatu kunatakiwa kufanyike vikao ambavyo vitajadili changamoto na kuhimizana uwajibikaji wa kazi kwa kila mfanyakazi juu ya majukumu yake”.


Akielezea suala la leseni kwa wauguzi hao alisema ni jambo la muhimu sana kwanza linamtambulisha kujulikana na yule anaetaka kumfanyia huduma ili iwe rashis kwake kutoa huduma.


Hata hivyo alifahamisha kwamba faida ya kuwa na lesini inakupunguzia matatizo na gharama  kwani hapo awali bei ya kawaida ilikuwa 40,000  na sasa 50,000  ambapo bei hiyo ni kwa muda na itarejea kama  ya awali na ilopita muda ya kurinyuu ni 50,000 .


Nao wauguzi hao wamewahidi viongozi wao kuyafanyia kazi maagizo walipewa ili kuona mabadiliko yanaongezeka zaid ya utendaji kazi na kutoa huduma kwa wananchi wao.

Comments