Admeli Sayyid Mahmoud Mousavi Jumapili
hii aliashiria namna vikosi vya majini vya Iran vilivyo na nguvu na
kueleza kuwa Iran ni nchi inayopakana na bahari na kwa msingi huo
inapasa kuwepo siku zote katika maji ya kimataifa.
Admeli Mousavi
amesema kuwa suala la kuwatuma wanajeshi wa majini katika bahari ya
Atlantic lipo pia katika ajenda ya kazi na kuongeza kuwa: Kuwepo
wanajeshi wa majini wa Iran katika bahari ya Atlantic kutafanyika
kulingana na wakati na pale itakapohitajika kwa mujibu wa mahitaji na
agizo la uongozi wa juu.
Kuhusu vikwazo vya kidhulma na vya
upande mmoja vya Marekani dhidi ya Iran, Naibu Kamanda wa oparesheni za
jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameeleza kuwa licha ya Jamhuri ya
Kiislamu ya Iran kuwekewa vikwazo kama hivyo vya kidhulma tangu mwanzoni
mwa Mapinduzi ya Kiislamu lakini hatua kwa hatua nchi hii imeweza
kupiga hatua kubwa za maendeleo.
Comments