Alisema hayo jana alipokuwa akiwahutubia wananchi katika kumbukizi ya
kuzaliwa Mtume Muhammad (SAW) inayofanyika kitaifa Wilaya ya Korogwe
jijini Tanga.
Alisema jambo la ushoga nchini halikubaliki na linapaswa kupingwa kwa nguvu zote.
“Jambo la ushoga halikubaliki, haiwezekani nchi tukufu kama Tanzania
kuwa na vitendo hivi, masheikh lisemeeni jambo hili ili tunusuru umma na
Taifa kwa ujumla,” alisema.
Baraza hilo limeongozwa na Waziri wa Nchi, Tamisemi, Selemani Jafo,
kwa niaba ya Rais John Magufuli na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa
dini na serikali.
Akizungumza katika baraza hilo, Jafo aliwaomba waislamu kuendelea
kumuombea Rais Magufuli ili aendelee kuwaletea maendeleo watanzania.
zanzibarleo.
Comments