Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara
baada ya kumaliza ziara ya kikazi kwa taasisi zikizopo chini ya wizara
hiyo yenye lengo la kuangalia utendaji wa kazi kwa wafanyakazi wa
taasisi hizo.
Alisema, katika taarifa zao zimemridhisha kuamini kuwa wamekuwa
wakifanya kazi ikiwemo kwa jeshi la polisi ambalo limeweza kudhibiti
uhalifu visiwani Zanzibar.
Alisema kwa mujibu wa ripoti, uhalifu unaendelea kupungua na
kudhibitiwa kwani ambapo kuanzia mwezi Januari hadi Oktoba mwaka huu,
ripoti ya uhalifu kwa vitendo vya uhalifu umepungua kwa asilimia 34
pamoja na makosa madogo yapo kwa asilimia wamepunguza na kudhibiti kwa
asilimia 57.
Aidha alisema takwimu hizo zinaonesha kuwa Zanzibar kumekuwepo kwa
mafanikio ambayo yamekuwa yakiendelea kupatikana katika kudumisha amani,
utulivu na usalama.
Hivyo, alimpongeza Kamishna wa Jeshi la polisi Zanzibar na watendaji
wake kwa kazi nzuri anayoifanya licha ya kuwepo kwa changamoto
zinazomkabili.
Akizungumzia taasisi ya Nida, alisema kuwa wamekuwa wakifanyakazi
nzuri na kufanikiwa malengo waliyojiwekea na kufanikiwa kwa asilimia 99
pamoja na kuweza kutoa vitambulisho hivyo kwa asilimia 90.
Kwa upande wa Uhamiaji, alisema kuwa wameweza kuendelea kudhibiti wa
uingiaji, utokaji na ukaazi wa wageni na kuweza kukamata wahamiaji
haramu, kufikishwa mahakamani na wengine kurudishwa walikotoka.
“Kwa kweli ni jambo la kupongezwa sana kwa watendaji wa taasisi hizi
mmeonesha moyo wa kufanyakazi, kwani hata uhalifu umepungua kwa asilimia
kubwa zaidi na upatikanaji wa huduma kupitia taasisi zenu zimekuwa
umeimarika”, alisema.
Hivyo aliwathibitishia wananchi kwamba wizara yake itaendelea
kudumisha amani, usalama na utulivu uliokuwepo sambamba na kuendeleza
ulinzi wa kudumu visiwani kupitia vyombo vya ulinzi vilivyopo chini ya
wizara hiyo.
Zanzibarleo.
Comments