Wavuvi hao walikamatwa jana Jumapili karibu na ufukwe wa Bamgot,
kando kando ya Ziwa Victoria.
Kamishna Mkuu wa Polisi kaunti ya Migori,
magharibi mwa Kenya, Joseph Nthenge amesema wavuvi hao wa Tanzania
wanazuilia katika kituo cha polisi cha Macalder na kwamba watapandishwa
kizimbani karibuni hivi, mara tu uchunguzi utakapokamilika.
Haya yanajiri wiki chache baada ya wavuvi 36 wa Kenya kukamatwa na
vyombo vya usalama vya Tanzania, kwa kuingia na kuvua katika maji ya
nchi hiyo katika Ziwa Victoria kinyume cha sheria.
Huko nyuma, wavuvi wa Kenya wamewahi kukamatwa pia na vyombo vya
usalama vya Uganda, wakikabiliwa na mashitaka kama hayo ya kuingia
katika maji na ardhi ya nchi hiyo kinyume cha sheria. Kenya na Uganda
kwa miaka mingi sasa zimekuwa zikizozania kisiwa cha Migingo, kilichoko
katika Ziwa Victoria.
Ieleweke kuwa, maji ya Ziwa Victoria yako ndani ya ardhi ya nchi tatu hizo za Afrika Mashariki, yaani Kenya, Uganda na Tanzania.
parstoday.
Comments