DC Micheweni:upo umuhimu wa kuanzisha SALAMA CUP.


  
 Mku wa wilaya ya Micheweni Mh. Salam Mbarouk Khatib amesema michezo nimuhimu katika kujenga afya za binadamu hivyo nivyema kila mmoja kuipa umuhimu wakipee.

Ameyasema hayo wakati akikabidhi Kombe la ujirani mwema kwa timu ya Combain iliyo ibuka kidedea dhiri ya Beach Boys katika michuano hiyo iliofanyika kiwanja cha maji maji Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema kutokana na umuhimu wa mchezo huo ulioipa hadhi kubwa Wilaya yake ameamua kutangaza michuano ya SALAMA CUPA ambayo itatoa motisha kwa timu za wilaya hiyo.

Alifafanua kuwa nifaraja kuona timu za wilaya ya micheweni kuipa umuhimu wa kuanzisha ligi zao wenyewe nakuahidi kama Kiongozi wa wilaya hawezi kubaki nyuma nakutangaza kutoa nguvu zaidi kupitia ligi itakayo anzishwa hivi karibuni ya salam cup.

“Nimejifunza mengi leo kutoka ndani ya mchezo huu na nikupongezeni timu zote zilizo shiriki Kombe la Ujirani Mwema pamoja na viongozi wote bila kujali mukaamua kulifanikisha hili” Alisema Salama.

“leo naomba nitangazieni ligi ambayo mimi mwenyewe nitaianzisha naipa jina la SALAMA CUP hii itazidisha mapenzi hasa kwa wilaya yetu”.

Katika mchuano kati ya Comban na Beach Boys ulimalizika kwa penalt zilizo ipa ushindi mkali timu ya Comban wa mabao 3 kwa 2 nakulazimisha kuwa washindi wa Kombe la Ujirani Mwema lilioanzishwa na Viongozi wa Jimbo la Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba.
Mh. salama akitoa maelekezo kwa wachezaji wa Beach Boys
Mh. salama Akimpatia maelekezo golkipa wa timu ya Beach Boys Juu ya kujenga heshima katika mchezo.
Mkuu wa wilaya ya micheweni Mh. Salama Mbarouk Khatib akikagua timu kabla ya mchezo kuanza.
Mkuu wa wilaya ya micheweni salama Mbarouk Khati akiwa na katibu tawala wa wilaya ndogo ja kojani kushoto.
Mkuu wa wilya ya Micheweni akisalimiana na wachezaji wa timu ya Combain.


Comments