Alisema hayo wakati akimjuilia hali Waziri wa zamani, Suleiman Othman Nyanga, nyumbani kwake Mpendae mjini Unguja.
Alisema zipo taratibu zilizowekwa na serikali kupitia wizara ya afya
za kumpatia uhamisho mgonjwa awe kiongozi au mwananchi wa kawaida wa
kupelekwa matibabuni Tanzania Bara au nje ya nchi iwapo hali ya afya
yake inakuwa mbaya asa kutokana na ukosefu wa vipimo au utaalamu.
Alimuhakikishia waziri huyo wa zamani wa Zanzibar kwamba serikali
itaendelea kumpa msaada wakati wowote pale atakapohitaji kulingana na
afya yake licha ya kupangiwa kurejea tena matibabuni nje ya nchini
mwanzoni mwa mwaka ujao.
Pamoja na mambo mengine viongozi hao pia walizungumzia hali ya soka
visiwani Zanzibar ambapo Balozi Seif akimkumbusha Nyanga enzi zake
wakati alipokuwa mchezaji wa kutegemewa wa timu ya soka ya Miembeni
wakati yeye akiwa kipa wa timu ya Ujamaa.
Zanzibarleo.
Comments