Watoa tiba asili watakiwa kukata vibali Pemba.

Related imageMkuu wa Baraza la Tiba asili na tiba mbadala Wizara ya afya Pemba Dk Shehe Omar Abdalla ,amewataka watu wanaojihusisha na masuala ya tiba za asili kukata vibali vya ufanyaji wa kazi zao ili kuweza kutambulika kisheria na baraza hili ili.kuweza kuepuka usumbufu utakao wafanya kushindwa kazi zao za kuwatibu wananchi kwa njia ya tiba asilia.

Alisema kuwa shughuli za utoaji wa matibabu kwa kutumia tiba asili ,matangazo ama kisomo bila ya kuwa na kibali ama leseni ya kuruhusiwa kufanya kazi hiyo  nikinyume na utaratibu kwa baraza la tiba asili ba tiba mbdala hapa Zanzibar.

Kauli hiyo ameitoa huko kijiji cha Raha Shehia ya Ukunjwi Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba wakati alipofika kumkamata Ibrahim Suleiman alokuwa akiendesha shughuli hizo za tiba asili kwa njia ya kisomo na kuwapatia dawa wagonjwa hao bila jambo ambalo ni makosa kwake kwani amekiuka  sheria ya baraza la tiba asili na tiba mbadala kwamba kila mtu anatakiwa kuwa na leseni ya kazi hiyo.

"Ndugu yetu Ibrahim hii ni mara ya pili kumkamata akiendesha shuguli za utoaji wa matibabu asilia kwa  kisomo cha cha kurani  katika mkusanyiko wa watu kinyume na sheria zetu na leo nimechukua nafasi hii ya kumkata na kumfikisha kituoni ili kumchukulia hatua za kisheria kwani amekua akikaidi magizo yetu" alisema .

Alifahamisha kitengo kinachoruhusu kufanya kazi hizo za tiba asili ni baraza la tiba asili na tiba mbadala  pekee na sio sehemu yenyengine yoyote wao ndio wanao husika na masuala hayo tu na kutoa mamuzi.

Aidha alifahamisha kuwa  sheria ya baraza la tiba asili na tiba mbadala limeweka faini kwa mtu yoyote ambae ata kamatwa akifanya kazi hiyo bila kibali kulingana biashara wenyewe na kazi ilivyo kwa kuanzia kiwango cha laki tatu na kwenda juu.

"Faini zetu zinategemea na kazi wenyewe kama alivyo ifanya ndg yetu Ibrahm faini yake yeye ni Shilingi laki tatu na nimemtaka akailipie benki pesa hiyo ili kuondokana na usumbufu kwenye kazi yake".alifahamisha.

Kwa upande wake mtoa huduma hiyo Ibrahim Suleiman ,alikiri kufanya kazi hiyo bila ya kuwa na kibali kinacho mruhusu kufanya kazi hizo na kumtaka Mkuu huyo wa baraza la tiba asili na tiba mbadala kumpunguzia faini hiyo  kwa vile amekubali kutenda kosa kinyume na sheria za baraza hilo.

Nae Mzee Khamis Said Ali, aliyekuwa akipatiwa huduma hiyo ya kisomo alisema alifika hapo kupatiwa dua kwani anasumbuliwa na matatizo ndani ya mwili wake na kusema mtibabu huyo anawadanyia tiba hiyo bila ya kuwatoza pesa kinyume na kauli za watu wanazosema kwamba anawadai Eflu Thalathini  baada ya kumaliza matibabu hayo.

Na mwandishi wetu.

Comments