wananchi waaswa kufua shria kuepuka madhara.


Image result for juma bakar alawiWananchi wa wametakiwa kuchukua tahadhari pindi watafiti wa gesi na mafuta watakapo anza zoezi la mionzi kwa ukanda wa bahari mara baada ya kukamilisha zoezi hilo kwa maeneo ya nchi kavu ili kuepuka madhara yanayoweza kuepukika.

Akizungumza na wananchi katika mkutano wa kutoa elimu juu ya utafiti wa mafuta na gesi huko Tumbe Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba Afisa mdhamini wizara ya ardhi, nyumba maji na nishati Juma Bakar Alawi amesema nivyema kwa wananchi kuwa na tahadhani kwani mionzi inayo toka katika zoezi hilo ina madhara kwa afya za binadamu.

Amefahamisha kuwa nivyema kwa wananchi kufuata miongozo itakayo tolewa wakati zoezi hilo litakapoa anza katika maeneo yanayo lengwa kuendeshwa tafiti hizo.

Amesema kuwa lengo la serekali si kumuonea mwananchi bali nikujaribu kutumia hekma ilikuona wanendelea kuishi katika hali ya usalama na amani bila athari zozote.

Sambamba nahayo amewataka wananchi kuwa wasikivu na kuwa walimu kwa wengine ilikuona mafanikio yanafikiwa bila kuwepo malalamiko yasio yalazima.

"najua wananchi sio wakaidi fuateni sheria  kwani miozi hiyo inananadhara kwa wanadamu basi tuambizane ili kuepuka madhara hayo."

Jumla ya shehia 30 zimepatiwa elimu uwelewa kabla ya zoezi hilo kuanza katika ukanda wa bahari kisiwani Pemba.

Comments