Walimu watakaowapa wanafunzi ‘home-work’ wakati wa likizo kukiona.

WIZARA ya Elimu nchini Kenya imewaonya walimu watakaowapa wanafunzi kazi za mazoezi kufanya nyumbani (home –work)  wakati wa likizo kubwa ya mwisho wa mwaka.

Skuli zote zilifungwa wiki iliyopita kwa ajili ya mapumziko ya Novemba – Desemba ambapo zinatarajiwa kufunguliwa Januari 2, 2019.

Mkurugenzi wa Elimu ya Sekondari, Paul Kibet alisema, Wizara imetoa mapumziko hayo ili kuwawezesha wanafunzi kuweza kujipumzisha na kujichanganya na jamii, sambamba na kuungana na familia zao na jamii ambazoo wanatokea.

“Ndio maana skuli zinashauriwa kutowapa wanafunzi wao kazi nyingi wanapokwenda nyumbani kwa ajili ya mapumziko. 

Iwapo watapewa kazi hizo wakiwa katika mzingira ya nyumbani itawazuia kujichanganya na maisha kikamilifu,” alisema  Kibet.


Zanzibarleo.

Comments