Maonyesho ya Kilimo yafanikiwa vyema Pemba.

Image result for maonesho a kilimo chamanangwe pembaWananchi kisiwani Pemba wameendelea kujitokeza kwa wingi na kuhamasika kwenda kushiriki maonyesho ya siku ya chakula duniani kwa Zanzibar yanaendelea katika mashamba ya chamnangwe wilaya ya wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Akizungumza katika eneo la maonyesho Afisa mdhamini wizara ya ardhi nyumba maji na nishati Zanzibar Juma Bakari Alawi amesema kiujumla wananchi wamehamasika kuweza kushiriki maonyesho hayo kikamilifu.

Amesema hiiyote nikutokana na waliowengi kuweza kuitikia wito wa serekali wakushirikia kikamilifu ili kujifunza mambo mbali mbali yanayopatikana katika maonyesho hayo ya siku ya chakula Duniani nao waweze kuyatumia baada ya kukamilika kwake.

Aidha amewataka wananchi na wajasiriamali kwaujumla kujifunza mbinu mbali mbali za kilimo ambazo zitawasaidia wao kuweza kuendana na kilimo cha kisasa ambacho kitaweza kutoa tatizo la njaa hapa nchi.

Omar Rashid Omar Afisa mkuu Idara ya Mipango na Utumishi Kutoka Wizara ya Kilimo Maliasili Mifugo na Uvuvi Pemba amesema wananchi wamekuwa wakijitokeza kwa wingi kujionea maonyesho hayo nakuweza kutoa michango yao ambayo yatawasaidia kuweza kuondoa changamoto ambazo zimeonekanwa.

Amefahanisha kuwa wananchi watambue maonyesho hayo sio yawizara ya Kilimo pekee baliniyakila mwananchi anayo fursa yakuweza kushiriki kikamilifu kwani yanaweza kuwaongezea uwelewa juu ya mazao yakilimo nayale yakibiashara.

Kwaupande wake Afisa masoko kutoka Benk ya Watu wa Zanzibar Asia Khamis Shaaban maesema maonyesho hayo yameweza kuwapa faraja kwao na kwanawananchi kwani walio wengi walikua hawajui matumizi sahihi ya kibank nao kuweza kutoa elimu hiyo kwalioweza kuhudhuria katika kibanda chao.

Nao baadhi ya wananchi waliopana nafasi yakutoa maoni yao wameitaka srekali kuyafanya maonesho hayo kuwa endelevu kila mwaka kwani yanatoa hamasa na mafunzo ambayo nayawasaidia kujikomboa kimaisha.

Kaulimbiu ya maonyesho hayo ni juhudi zetu ndio hatma zetu dunia bila njaa inawezekana ifikapo mwaka 2030.

Comments