Kamanda Mambosasa Atoa Onyo kwa Bodaboda Dar....60 Watiwa Mbaroni Kwa Kuhujumu Shirika la Umeme Tanzania(Tanesco).
Jeshi
la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema limeanza operesheni
maalumu ya kukamata bodaboda zote zinazoingia katikati ya Jiji ambapo
ndani ya saa 24 wamekamata pikipiki 104.
Hayo
yamesemwa jana na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Lazaro Mambosasa wakati anazungumza na waandishi wa habari kuhusu
operesheni ambazo wanazifanya.
Alisema
Polisi wameanza operesheni ya kukamata waendesha bodaboda ambao
wanaingia katikati ya mji wakati wamezuiliwa kuingia mjini.
Kamanda
Mambosasa alisema baadhi ya bodaboda ambazo zimekamatwa zimetokana na
makosa ya kutovaa kofia ngumu kwa wanaoendesha,kupitia njia tofauti na
utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria na kupakia mishikaki.
"Ni
marufuku bodaboda kuingia katikati ya Mji,hatuwezi kuacha hilo
likaendelea kufanyika.Walishakatazwa kuingia katikati ya mji." Alisema
Mambosasa na kuongeza;
"Mbali
ya kuwakamata wanaiongia mjini pia tunaendelea na operesheni ya
kukamata bodaboda ambazo zinatumika kutenda matukio ya uhalifu.Pia
tutakamata bodaboda ambazo wanaoziendesha wanashindwa kufuata sheria za
usalama barabarani."
Wakati
huo huo Mambosasa amesema Polisi kwa kushirikiana na Shirika la Umeme
Tanzania(Tanesco) wamefanikiwa kukamata watu 60 ambao wanatuhumiwa
kujihusisha na kuhujumu miundombinu ya umeme na kujiunganishia umeme
bila utaratibu na kuchezea mita za Luku.
Kamanda
Mambosasa alisema wapo ambao wamefikishwa mahakamani na wengine
wanaendelea kuhojiwa na kisha watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma
hizo.
Alisema
kuwa wanaojihusisha na kuhujumu miundombinu ya umeme wafahamu
opereshenii hiyo ni endelevu na kwamba watakaoendelea wajue wao ni
wafungwa watarajiwa kwani hawatabaki salama.
Mpekuzi.
Comments