Balozi Seif : Wananchi limeni muhogo kwa wingi kuweza kufikia malengo ya soko la China.

Makamo wa pili wa rais Mh. balozi Seif ali Iddi amewataka wananchi kisiwani Pemba kulima zao la mihogo kwa wingi ili kuendana na mahitaji ya soko nchini china.
Akufunga maonyesho ya siku ya chakula duniani huko chamanangwe Mkoa wa Kasakazini Pemba amesema Tanzania imepata fursa kubwa yakupeleka muhogo nchini china fursa ambayo nchi nyingi hawakuipata.
Ameeleza kuwa nimuda sasa kwa wakulima wa muhogo kuweza kulishughulikia zao hilo ili liweze kuwakomboa na halingumu za kinmaisha.
Katika hatua nyengine Balozi Seif amewataka vijana kuachana na tabia ya kusubiri kuajiriwa na serekali na badalayake kuitumia sekta ya kilimo kama mkombozi wa tatizo la ajira nchini.
Nae naibu waziri wizara ya kilimo maliasili mifugo na uvuvi Dr. makame Ali Ussi amewashukuru wajasiriamali kwa kushiri kikamilifu katika kufanikisha maonyesho hayo ambayo yamefanikiwa kwa kiasi kikumbwa.
Maonesho ya siku ya chakula duniani yalifunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Dr. Ali Mohd shein Na kufungwa na Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar Mh. Balozi Seif Ali Iddi na yamegharimu Jumla ya Tsh milioni 140 amapo kaulimbiu ya maonyesho hayo ni Juhudi zetu Ndio Hazina Yetu Dunia bila njaa inawezekana ifikapo mwaka 2030.

Comments