ADA-TADEA yaunga mkono kauli ya Ras Al Khaimah.

KAULI ya mtawala wa Ras al Khaimah, Sheikh Saud Bin Saqr Al-Qasimi, juu ya kuhakikisha watu wa Zanzibar wanaendelea, imeungwa mkono na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ADA TADEA, Juma Ali Khatib, akisema imetoa matumaini kwa wanachi wa Zanzibar.
Hayo aliyasema wakati akizungumza na Zanzibar Leo, mara baada ya utiaji saini mkataba wa mgawanyo wa uzalishaji wa mafuta na gesi.
Mkataba huo ulisainiwa juzi saa 1:57 usiku kati ya Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Maendeleo ya Mafuta Zanzibar (ZPDC), Mwanamkaa Abdulrhaman Mohamed na Mohamed Ataya, kutoka kampuni ya RAKGAS ya nchini Ras al Khaimah.
Utiaji saini huo ulishuhudiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na Mtawala wa Ras al Khaimah, Sheikh Saud Bin Saqr Al Qasimi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idi, Mawaziri wa SMZ na wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na viongozi wa chama.
Alisema kitendo chake cha kutoonesha upendeleo wa kutoa huduma muhimu katika jamii ya Wazanzibari, kimeonesha anavyowajali.
Alisema chama chao kimepokea kwa furaha tamko la kiongozi huyo kwani limewaonyesha njia ya kuwa na Zanzibar yenye maendeleo.
Zanzibarleo.

Comments