Waziri Mkuu kuongoza mazishi waliofariki dunia kwenye kivuko cha MV Nyerere....Hadi Sasa Idadi Imefika 225.
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwasili katika kijiji cha Bwisya
Kisiwa cha Ukara kuongoza ibada ya mazishi ya baadhi ya watu waliopoteza
maisha katika ajali ya Kivuko cha MV Nyerere iliyozama Septemba 20,
2018.
Akizungumza
leo Jumapili Septemba 23, 2018 mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella
amesema kiongozi huyo atajumuika na viongozi wengine ambao wapo kisiwani
hapa kushiriki mazishi ya miili ambayo haijatambulika na ambayo ndugu
wameomba izikwe kwa utaratibu ulioandaliwa na Serikali.
Zaidi
ya miili 225 imeopolewa, miili 172 kutambuliwa na 112 imechukuliwa na
ndugu kwa ajili ya mazishi huku 37 ikiwa haijatambuliwa hadi leo
asubuhi.
Mpekuzi.
Comments