
Mkurugenzi wa idara ya misitu na rasilimali zisizorejesheka
Soud Moh’d Juma amesema kuna baadhi ya watendaji wamekuwa si waadilifu na hushirikiana
na wahalifu kwa kuharibu rasilimali na mazao ya misitu hiyo kitu ambacho
kinaondoa haiba ya misitu hiyo.
Soud ameyasema hayo huko msitu wa Ngezi Kisiwani Pemba katika
kikao cha pamoja kati wakuu wa idara ya misitu na wafanyakazi wa msitu huo.
Pamoja na hayo Mkurugenzi huyo amesema umefika wakati sasa
kwa kila mhudumu wa hifadhi kutekeleza majukumu yake kwa vitendo ikiwemo kuandika
taarifa za kazi alizozifanya kwa kutwa ili kuepukana na uhalifu huo.
Nao baadhi ya wafanyakazi hao wamesema wamekuwa wakikabiliwa
na changamoto mbalimbali katika utekelezaji
wa shughuli zao ikiwemo kutokuwa na silaha, sare na vitambulisho vya kazi ambapo
baadhi yao wamefika kuitishiwa usalama wao katika hatakati zao za doria.
Comments