Baada
ya ndege yake kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa John F.
Kennedy, Rais Rouhani ambaye alikuwa amezungukwa na waandishi wa habari
alisema kuwa, mazingira ya sasa ya Marekani yanaonekana tofauti na ya
miaka iliyopita na kwamba Wamarekani wamerudi nyuma na kujiondoa katika
mikataba kadhaa ya kimataifa ikiwa ni pamoja na mkataba wa nyuklia wa
JCPOA.
Safari ya Rais Rouhani nchini Marekani imefanyika siku moja baada ya
shambulizi la kigaidi lililofanyika katika mji wa Ahvaz, kusini mwa Iran
na kuua makumi ya watu wasio na hatia.
Kabla
ya kuuondoa Tehran, Rais Rouhani alisema kuwa Marekani inafanya
mikakati ya kuvuruga usalama na amani nchini Iran kwa msaada wa viinchi
vidogo mamluki na kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imejipanga vizuri
kukabiliana nao.
Akizungumzia
shambulizi la kigaidi la juzi mjini Ahvaz, Rais Rouhani amesema:
"Tunawajua waliofanya shambulizi hilo, ni kina nani na wanafungamana na
nani."
Amesema Marekani ndiyo inayozipa himaya na misaada nchi ndogo na
mamluki wake na kuwachochea kufanya uhalifu na jinai kama hizi.
parstoday.
Comments