Epukeni udanganyifu wakati mukisafirisha mizigo yenu.


Image result for wafanyabiashara pembaWafanyabiashara kisiwani Pemba wametakiwa kulipa kodi kwa wakati nakuepuka udanganyifu pindi wanapo safirisha mizigo yao kutoka sehemu moja kwenda nyengine.

Hayo yamesemwa na Afisa mdhamini wizara ya Fedha nd. Ibrahim Saleh Juma wakati alipokuwa akizungumza na wafanyabiasha wa mkoa wa kusini Pemba katika semina ya sikumoja juu ya marekebisho ya Sheria kwa mlipa kodi huko katika ukumbi wa baraza la mji chake chake.

Amesema kumekuwepo na baadhi ya wafanyabiasha ambao hutoa taarifa za uongo jambo ambalo linaleta usumbufu mkubwa wakati wa ulipaji wa kodi.

Amefahamisha kuwa nivyema kwa wafanyabiashara hao kuwa waaminifu pindi wanapo wasilisha vielelezo vyao kwa bodi ya mapato Zanzibar ZRB ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa zao kiukamilifu.

Aidha amewakumbusha wafanyabiashara hao kuwa na utaratibu wa kujiwekea kumbu kumbu ili ziwarahisishie wao na wakaguzi wanapofika kutafuta takwimu hizo.

Akiwasilisha mada ya mabadiliko ya sharia zilizo fanyiwa marekebisho Mwanasheria wa Bodi ya mapato Zanzibar ( ZRB ) Khamis Jafar Mfaume amewataka wafanya biashara hao kuzielewa vyema sharia hizo ili kuepuka malamiko yasio yalazima wakati wa ulipaji wa kodi.

Amesema kuwa lengo la kurekebishwa kwa sharia hizo nikuondoa changamoto zinazojitokea kwa walipa kodi ili ziweze kutekelezwa kwa muda muafaka na bila pingamizi.

Akizitaja sharia zilizo fanyiwa marekebisho kuwa ni pamoja na Sheria ya Usimamizi wa kodi, Sheria ya ushuru wa Stamp, Sheria ya kodi za mafuta na Sheria ya rufaa ya Kodi.

Kwaupande wao wafanya biasharao hao wameitaka Serekali ya mapinduzi Zanzibar kupitia Bodi ya mapato ZRB  kuwasimamia kikamilifu wafanya biashara wote wanokwepa ulipaji wa Kodi ili kuweza kuleta maendeleo nchini.

Comments