Afisa mdhamini wizara ya maji, ardhi nyumba na nishati atoa neno kwa wananchi wa Mfikiwa Chake chake Pemba.

Amesema hakuna sababu kuona baadhi ya watu wanakwamisha harakati hizo ikiwemo ujenzi wa barabara na
mambo mengine na kusababisha mivutanao
isiyo na ulazima.
Ameyasema hayo huko
katika shamba la mivinje Mfikiwa Chake
chake linalomilikiwa na Nassor Moh’d Issa
katika kulifanyia tathmini ya thamani ya mali zilizomo ili kupisha
ujenzi wa barabara kwenye eneo la Polisi Mfikiwa.
Afisa mdhamini huyo amesema mizozo katika kuleta maendelo
haileti tija hivyo ni budi kwa wamiliki wa rasilimali na taasisi kukubaliana na
kuondoa tofauti zao ili kazi iendelee kama ilivyopangwa.
Katika hatua hiyo Sheha wa Shehia ya Mfikiwa Bimkubwa Rajab
Tangwi amesema chanzo cha mzozo huo kilitokana na mmiliki wa shamba hilo kukataa
kukubaliana na tathmini ya awali ya shilingi milioni tisa huku mwenyewe
akihitaji milioni 35.
Naye mwakilishi wa mmiliki mwenye shamba hilo la Mivinje Said
Moh’d Issa amesema ameridhishwa na tathmini ya sasa lakini kauli sahihi iko kwa
mwenye mali ambaye yuko Tanzania bara.
Shamba hilo la mivinje liko kwenye kona mbaya na meneja wa ujenzi wa barabara hiyo Amini
Khalid Abdalla amesema lazima waondoe sehemu ya miti hiyo ili barabara iweze kuwa bora na kiwango
kinachokubalika kwa usalama wa watumiaji wa barabara hiyo .
Comments