Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof.
Adolf Mkenda amefanya mazungumzo na kampuni ya Burmeister &
Partiners (PTY) LTD ya nchini Namibia tarehe 10 Agosti 2018 mjini
Windhoek, Namibia.
Akiongea
na uongozi wa kampuni hiyo Prof. Mkenda alieleza Tanzania ina eneo
kubwa la ardhi yenye rutuba ambayo haitumiki na rasilimali watu ya
kutosha hivyo ni fursa kwa mwekezaji mwenye nia thabiti kuwekeza nchini.
“Lengo
la Serikali ni kupata mwekezaji aliye makini kama wewe nimeona una
mradi mkubwa wa shamba la mifugo na vifaa vya kisasa kwa ajili ya
machinjio nina imani ukija kuwekeza Tanzania hautajutia kabisa kwakuwa
matumizi ya teknolojia ya kisasa katika miradi itaongeza thamani ya
mazao na bidhaa zitakazozalishwa na kuwezesha kupatikana kwa soko la
kimataifa” alisema Prof. Mkenda
Naye
Mkurugenzi wa kampuni hiyo Mhandisi Hendrik Boshoff alieleza kampuni
imekuwa ikifanya kazi katika mataifa mbalimbali ambapo kampuni hiyo
imefungua kampuni ya maziwa nchini Rwanda ambayo inauza na kusafirisha
mataifa mengine pia imewekeza nchini Angola katika miradi ya uvuvi na
imekuwa ikifanya vizuri katika biashara zake zote.
Pia
alisema kampuni imebobea katika miradi ya ujenzi, nishati, miradi ya
maji, usafiri, usanifu majengo, ujenzi wa majengo, miradi ya machinjio,
mashamba ya mifugo na pia ipo katika mpango wa kuanzisha miradi ya
viwanda vya dawa za binadamu ambapo utekelezaji wake utaanza mara baada
ya kukamilisha mazungumzo na wataalamu kutoka nchini Cuba.
Prof.
Mkenda alieleza miradi yote kutoka katika kampuni hiyo inatija kubwa
kwa maendeleo ya taifa la Tanzania hivyo akaikaribisha kampuni hiyo kuja
mapema nchini ili kuweza kujionea rasilimali zilizopo na kuainisha
miradi watakayoweza kuanza nayo. Vilevile akaeleza kampuni hiyo ina
nafasi ya kutumia fursa za mji wa Dodoma katika uwekezaji kufuatia
kuhama kwa mji wa Serikali kutoka Dar es Salaam.
Kampuni
ya Burmeisters & Partiners (PTY) LTD ilianza kufanya kazi zake
nchini Namibia mwaka 1984 na baadae kuwa miongoni mwa kampuni kubwa
zilizowekeza nchini humo. Pia ni kampuni hiyo inatoa huduma za
kihandisi na huduma za usimamizi wa miradi katika taaluma mbalimbali.
Mpekuzi.
Comments