Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.
Selemani Jafo, amewataka Maafisa Kilimo kuhakikisha kuwa wanaendelea
kutoa utaalamu wa kilimo katika mabanda ya Nanenane hata baada ya
maonesho hayo kukamilika ili wananchi waweze kufaidi utaalamu wao
Aliongeza
kuwa ipo haja kwa kila kanda kunapofanyikia maonesho ya Nanenane
kuandaa wataalamu wa kilimo ambao watakuwa wakiendelea kutoa huduma hizo
hata baada ya maonesho hayo kumalizika
Waziri
Jafo alitoa kauli hiyo jana kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika
kitaifa mkoani Simiyu, kabla ya kuzindua mwongozo wa namna ya kuandaa
mipango ya kilimo ya wilaya (District Agricultural Development Plans
Guideline- DADPs Guideline).
Alisema
kuwa mwaka jana akiwa jijini Dodoma aliagiza kuwa wataalamu wa kilimo
hawana budi kuwa na watumishi wa kudumu katika vibanda vya maonesho ili
waweze kutoa utaalamu wao kwa wananchi wanaohitaji huduma hiyo.
“Wakulima
wetu hawapaswi kungoja msimu wa Nane Nane ndio waje kujifunza mbinu na
maarifa ya ukulima bora ambao utakuwa na manufaa kwao bali inatakiwa
kila mkulima anapotaka kujifunza ajue lipo eneo ambapo anaweza kwenda na
kupata ushauri nasaha juu ya jambo linalo mtatiza katika Mifugo, Kilimo
au Uvuvi” alisema Jafo.
Mhe.
Jafo alisema asilimia 65 ya malighafi za viwanda hutokana na mazao ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi hivyo suala la wananchi wanaofanya shughuli hizo
kuwa endelevu halina budi kuzingatiwa na kupewa kipaumbele.
“Tunapoendelea
na Kampeni ya Kiwanda changu mkoa wangu ambapo tumeonekana kufanya
vizuri katika robo ya kwanza na kufikia asilimia 49 ya malengo ya kuwa
na viwanda 100 kwa kila mkoa lazima tujidhatiti katika kutoa utaalam wa
kutosha kwa wakulima wetu,” alisema Jafo.
Mbali
na uzinduzi wa mwongozo wa kilimo wa wilaya, Mhe. Jafo pia alikagua na
kujionea shughuli mbali mbali zinazoendelea katika kanda hiyo
inayounganisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na kujionea Vipando
kutoka Halmashuri za Mikoa hiyo, Mabanda ya Biashara sambamba na
kujionea shughuli ndogo ndogo za wajasiriamali zikiwepo shughuli za
usindikaji.
Waziri
huyo mwenye dhamana na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa alifanikiwa
pia kutembelea Banda la Wizara yake pamoja na taasisi zilizo chini ya
Wizara yake kisha kuwapongeza kwa namna wanavyo toa huduma kwa wananchi.
“Niwape
pongezi kwa kweli kwa kazi kubwa mnayofanya, wingi wa watu wanaowafikia
kutaka ufafanuzi wa masuala mtambuka ni ishara kwamba wananufaika na
elimu mnayowapa hivyo endeleeni kutoa huduma,” alisema Waziri Jafo.
Mapema
kabla ya kuzindua mwongozo huo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa
Kisekta kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa bwana
Leo Martin Mavika alieleza kuwa mwongozo huo unalenga kuelezea hatua
kwa hatua namna ya kushirikisha wananchi na wadau mbalimbali katika
kuandaa mpango wa maendeleo ya kilimo wa kijiji.
Aliongeza kuwa mwongozo huo pia unalenga kuunganisha mipango ya vijiji katika kata na hatimaye kupata mpango wa wilaya.
Bwana
Mavika alisema kuwa mwongozo huo utatumika katika kuandaa mipango ya
kilimo kuanzia mwaka wa fedha 2019/20. Kabla ya kufikia kipindi hicho
timu ya uwezeshaji wa taifa itatoa mafunzo ya namna ya kutumia mwongozo
huo kwa mikoa na halmashauri zote Tanzania
Maonesho
ya Nane Nane ya 2018 yanafanyika mkoani Simiyu na yanabebwa na
kaulimbiu “Wekeza katika Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa Maendeleo ya
Viwanda.
Mpekuzi.
Comments