KAIMU
Mkurugenzi wa Benki ya Kilimo(TADB) Japheth Justine ameshauri
Watanzania kujikita kwenye kilimo kwani kinalipa huku akifafanua wao
wapo tayari kutoa fedha asilimia 80 kwa wanaohitaji kukopa matrekta na
asilimia 20 iliyobaki itatolewa na mnunuzi.
Akizungumza
jana wilayani Kibaha mkoani Pwani mbele ya Katibu Mkuu wa Wizara ya
Fedha na Mipango Dotto James , Mkurugenzi wa TADB Justine alifafanua
kikubwa ambacho wanataka kuona ni mkulima kufanikiwa kupitia mazao yake
na ndilo miongoni mwa jukumu lao.
Akifafanua
zaidi Justine amesema wameshatoa mkopo wa Sh.bilioni 41.1 tangu
kuanzishwa kwa benki hiyo na wapo kwenye mikoa mitatu ambayo ni Dar es
Salaam, Mwanza na Dodoma na siku za karibuni watafungua tawi lingine
mkoani Mbeya na lengo lao ni kuwafikia wananchi kokote walipo
Pia
alisema wameshafanya makubaliano na Shirika la Maendeleo la Taifa(NDC)
kwa lengo la kusaidia wale wanaonunua matrekta kwamba benki ya kilimo
itaingiza asilimia 80 ya mkopo na mnunuzi atatoa asilimia 20.
Aliongeza
kwamba wakulima wamefanya vizuri kwenye zao la pamba huku akielezea
lengo lao ni kuchoche hamasa kwenye kilimo na kubwa zaidi ni kumuondoa
mkulima kwenye jembe la mkono.
“Pale
ambapo tutafanikiwa kumtoa mkulima kwenye jembe la mkono na kumpa
mashine ambazo zitamsaidia kuongeza tija na kumpa faida hicho ndicho
ambacho tunakihitaji.
“Kilimo
au mkulima ni muwekezaji na hivyo tunataka kuona mkulima anapata faida
.Hivyo kwa wakulima waliokuwa kwenye bodi ya pamba watapa mkopo wa
asilimia 80,”alisema.
Ameongeza
wataanza na matrekta 500 ambayo hiyo itafanyika muda si mrefu kwa
kuwapa wakulima waliofanya vema kwenye kilimo cha pamba.
Justine
alisema mpango wao mkubwa ni kwenda kuziambia benki za biashara
kuingiza asilimia 50 na wao wataweka asilimia 50 katika kumkopesha
mkulima.
Pia
alisema wanaishukuru Serikali kwa kuzindua mpango wa pili kwenye sekta
ya kilimo na watahakikisha wanafanikisha malengo ya Serikali.
Alisema
benki ya kilimo itahakikisha inawakopesha wakulima kwa bei nafuu na
kusisitiza kuwa kilimo kinalipa na hivyo Watanzania wajikite kwenye
kilimo.
Alisisitiza
wameanza na wakulima wa pamba katika kutoa hiyo asilimia 80 na iwapo
mpango huo utafanikiwa basi watakwenda kwenye maeneo mengine.
Kwa
upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango , James
amempongeza Mkurugenzi huyo wa benki ya kilimo kwani tangu alipoteuliwa
na Rais amesimamia mambo mengi aliyoagizwa kuyafanya.
Alisema kwa sasa benki hiyo ina fedha za kutosha kwa ajili ya kuwasaidia wakulima nchini.
Mpekuzi.
Comments