Ikiwa
ni siku chache tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John
Magufuli kutoa maagizo kwa viongozi kuwajibika na wasisubiri hadi
mwenyewe awawajibishe na kutolea mfano wa ajali zilizofuatana jijini
Mbeya.
Alfajiri
ya leo Julai 5, 2018, Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani Kanda Maalum
Dar es salaam kimezindua Operesheni ya Ukaguzi wa magari, madereva,
leseni na vyeti vya udereva kwa madereva wa mabasi ya Mikoani katika
stendi kuu ya Ubungo .
Zoezi
hilo limeongozwa na Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es
salaam, Liberatus Sabas, ambapo amesema kuwa lengo la operesheni hiyo ni
kuwafanya madereva kuacha tabia ya kughushi leseni, kuwahimiza
wajiunge na mafunzo ya udereva katika vyuo vinavyotambulika na serikali.
“Polisi
Kanda Maalum Dar es salaam inawataka Madereva wasio na leseni halali,
madereva walevi, pamoja wamilki wa magari walio na magari mabovu
kutoyaruhusu magari hayo kuingia barabarani hadi yatakapotengenezwa na
kukaguliwa”, amesema Kaimu Kamanda.
Kamanda
ameongeza kuwa Jeshi la Polisi halitasita kuchukua hatua kali za
kisheria kwa wamiliki, Madereva na Kampuni za usafirishaji zitakazoenda
kinyume na sheria, kanuni na taratibu za usalama
Mpekuzi.
Comments