Alisema kuwa ili kujiepusha na tishio hilo, serikali imeanzisha
tamasha la Mzanzibari ambalo pamoja na mambo mengine, ni chombo cha
kuulinda na kuuendeleza utamaduni huo kwa kukumbusha na kurejesha jamii
wapi inatoka.
Balozi Seif alitoa kauli hiyo jana wakati alipokuwa akifungua rasmi
tamasha la 23 za utamaduni wa Mzanzibari, kwenye viwanja vya Mapinduzi
Square Kisonge, ambapo hutuba yake ilisomwa kwa niaba ya Waziri wa
Habari, Utalii na Mambo ya Kale Mahmoud Thabit Kombo.
Alisema kuwa jamii yenye kubeza utamaduni wake hutumbukia kwenye
shimo la mtafaruki, jamii hiyo hukosa utambulisho ambao ni sawa na
bidhaa inayouzika sokoni kwa bei ya juu kabisa, na kama mipango
madhubuti itaandaliwa jamii inaweza kustawishwa kwa kutumia utamaduni
wa Kizanzibari.
Alisema kuwa ustarabu wa Zanzibar ni matokeo ya utamduni ambao
umeijengea sifa kubwa tangu zama za kale, na historia mbali mbali
imeandikwa juu ya jambo hili, ambapo watu kutoka mataifa ya Ulaya, Asia
na hata Afrika hutembelea Zanzibar na wengine kuamua kufanya maskani
yao.
Zanzibarleo.
Comments